< Isaya 13 >
1 Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:
La palabra del Señor acerca de Babilonia que vio Isaías, el hijo de Amoz.
2 Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu, wapazieni sauti, wapungieni mkono waingie katika malango ya wenye heshima.
Pon una bandera en la cima de una montaña, alza un grito fuerte, da instrucciones con la mano, para que puedan entrar por las puertas de los nobles.
3 Nimewaamuru watakatifu wangu; nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu: wale wanaoshangilia ushindi wangu.
He dado órdenes a mis consagrados, he enviado a mis hombres de guerra, los míos que se enorgullecen de mi gloria, para que den efecto a mi ira.
4 Sikilizeni kelele juu ya milima, kama ile ya umati mkubwa wa watu! Sikilizeni, makelele katikati ya falme, kama mataifa yanayokusanyika pamoja! Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.
¡El ruido de grandes números en las montañas, como el ruido de un pueblo fuerte! ¡El ruido de los reinos de las naciones reunidas! El señor de los ejércitos está ordenando sus fuerzas para la guerra.
5 Wanakuja kutoka nchi za mbali sana, kutoka miisho ya mbingu, Bwana na silaha za ghadhabu yake, kuangamiza nchi yote.
Vienen de un país lejano, de la parte más lejana del cielo, incluso el Señor y los instrumentos de su ira, con destrucción por toda la tierra.
6 Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu, itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
Envía un grito de dolor; porque cerca está el día del Señor; viene como destrucción del Altísimo.
7 Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
Por esta causa, todas las manos serán débiles, y todo corazón del hombre desfallecerá;
8 Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.
Sus corazones estarán llenos de temor; Dolores y penas los vencerán; Estarán sufriendo como una mujer en el parto; se sorprenderán el uno del otro; sus rostros serán como llamas.
9 Tazameni, siku ya Bwana inakuja, siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali, kuifanya nchi kuwa ukiwa na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.
Mira, el día del Señor viene, cruel, con ira y ardiente furor; convertirá de la tierra un desierto, llevando a los pecadores a la destrucción.
10 Nyota za mbinguni na makundi ya nyota havitatoa mwanga wake. Jua linalochomoza litatiwa giza na mwezi hautatoa nuru yake.
Porque las estrellas del cielo y sus ejércitos brillantes no darán su luz: el sol se oscurecerá en su viaje por el cielo, y la luna retendrá su luz.
11 Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake, waovu kwa ajili ya dhambi zao. Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi, na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.
Y enviaré castigo al mundo por su maldad, y a los pecadores por sus malas acciones; y pondré fin a todo orgullo, y abatiré el poder de los crueles.
12 Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi, watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.
Haré que los hombres sean tan pequeños en número, que un hombre será más difícil de conseguir que el oro, incluso el mejor oro de Ofir.
13 Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke, nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika siku ya hasira yake iwakayo.
Por esta causa temblarán los cielos, y la tierra se moverá de su lugar, en la ira del Señor de los ejércitos, y en el día del furor de mi ira.
14 Kama swala awindwaye, kama kondoo wasio na mchungaji, kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.
Y será que, como una gacela huyendo, y como ovejas errantes, irán cada uno a su pueblo y a su tierra.
15 Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo, wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.
Todos los que sean adelantados tendrán una lanza atravesada por él, y todos los que huyan serán arrojados a la espada.
16 Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande mbele ya macho yao; nyumba zao zitatekwa na wake zao watatendwa jeuri.
Sus hijos pequeños serán estrellados contra el suelo delante de sus ojos; sus bienes serán saqueados, y sus esposas serán violadas.
17 Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao, ambao hawajali fedha wala hawafurahii dhahabu.
Mira, estoy manejando a los medos contra ellos, que no le dan valor a la plata y no tienen placer en el oro.
18 Mishale yao itawaangusha vijana, hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga wala hawataangalia watoto kwa huruma.
En sus manos hay arcos y lanzas; son crueles, matan violentamente a los jóvenes y aplastan a los recién nacidos; no tienen piedad por los niños.
19 Babeli, johari ya falme, utukufu wa kiburi cha Wababeli, itaangushwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
Y Babilonia, la gloria de los reinos, la hermosa ciudad que es el orgullo de los caldeos, será como la destrucción de Dios de Sodoma y Gomorra.
20 Hautakaliwa na watu kamwe wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko, hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.
La gente nunca volverá a vivir en ella, y no tendrá más hombres de generación en generación: el árabe no levantará su tienda allí; y los que cuidan ovejas no lo harán un lugar de descanso para sus rebaños.
21 Lakini viumbe wa jangwani watalala huko, mbweha watajaza nyumba zake, bundi wataishi humo nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.
Pero las bestias del desierto tendrán sus agujeros allí; y las casas estarán llenas de lechuzas, y los avestruces tendrán su lugar allí, y los chivos retozaran allí.
22 Fisi watalia ndani ya ngome zake, mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari. Wakati wake umewadia, na siku zake hazitaongezwa.
Y los lobos se responderán unos a otros en sus torres fortificadas, y los chacales en sus lujosos palacios: su tiempo está cerca, y sus días de poder se terminarán rápidamente.