< Isaya 13 >
1 Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:
Vision d'Isaie, fils d'Amos, concernant Babylone.
2 Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu, wapazieni sauti, wapungieni mkono waingie katika malango ya wenye heshima.
Faites flotter l'étendard sur la montagne de la plaine; élevez la voix vers eux, appelez-les de la main; princes, ouvrez vos portes.
3 Nimewaamuru watakatifu wangu; nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu: wale wanaoshangilia ushindi wangu.
C'est moi qui les commande, c'est moi qui les conduis; des géants viennent assouvir ma colère, pleins de joie et d'insolence.
4 Sikilizeni kelele juu ya milima, kama ile ya umati mkubwa wa watu! Sikilizeni, makelele katikati ya falme, kama mataifa yanayokusanyika pamoja! Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.
On entend sur les montagnes la voix de maintes nations; et la voix de ces rois et de ces nations ressemble à celle d'une multitude assemblée. Le Seigneur des armées a donné ses ordres à une nation belliqueuse,
5 Wanakuja kutoka nchi za mbali sana, kutoka miisho ya mbingu, Bwana na silaha za ghadhabu yake, kuangamiza nchi yote.
Afin que le Seigneur et ses belliqueux combattants vinssent d'une terre lointaine et des extrémités du monde pour détruire toute la terre.
6 Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu, itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
Pousses des cris de douleur; car il est proche le jour du Seigneur, où cette destruction viendra de Dieu.
7 Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
C'est pourquoi toute main sera énervée, et toute âme aura peur.
8 Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.
Les anciens seront dans le trouble, et ils souffriront des maux comme ceux d'une femme qui enfante; et ils se regarderont l'un l'autre dans une même douleur; et ils seront hors d'eux-mêmes, et ils changeront de visage comme saisis par le feu.
9 Tazameni, siku ya Bwana inakuja, siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali, kuifanya nchi kuwa ukiwa na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.
Car le voilà qui vient le jour du Seigneur, inévitable, plein de vengeance et de colère, pour rendre la terre déserte et en détruire les pécheurs;
10 Nyota za mbinguni na makundi ya nyota havitatoa mwanga wake. Jua linalochomoza litatiwa giza na mwezi hautatoa nuru yake.
Car les astres du ciel, Orion, toute la splendeur céleste, ne donneront plus de lumière; et le soleil levant sera voilé de ténèbres, et la lune ne donnera plus sa clarté.
11 Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake, waovu kwa ajili ya dhambi zao. Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi, na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.
Et je punirai les méfaits de toute cette terre et les iniquités de ces impies; et je détruirai l'orgueil des pécheurs, et j'humilierai l'orgueil des superbes.
12 Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi, watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.
Et ceux qui resteront seront plus rares que l'or naturel, et un de ces hommes sera plus rare que la pierre d'Ophir.
13 Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke, nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika siku ya hasira yake iwakayo.
Car le ciel sera irrité, et la terre ébranlée dans ses fondements par la colère terrible du Seigneur des armées au jour où surviendra sa colère.
14 Kama swala awindwaye, kama kondoo wasio na mchungaji, kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.
Et ceux qui resteront fuiront comme un jeune chevreuil, comma une brebis errante, et nul ne sera là pour les réunir; et chacun retournera chez son peuple, chacun s'enfuira dans son pays.
15 Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo, wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.
Quiconque sera surpris seul sera opprimé, et ceux qui seront réunis périront par le glaive.
16 Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande mbele ya macho yao; nyumba zao zitatekwa na wake zao watatendwa jeuri.
Et sous leurs yeux on écrasera leurs enfants; on pillera leurs maisons, on violera leurs femmes.
17 Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao, ambao hawajali fedha wala hawafurahii dhahabu.
Voici que je vais susciter contre vous les Mèdes, qui comptent pour rien l'argent, et n'ont pas besoin d'or.
18 Mishale yao itawaangusha vijana, hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga wala hawataangalia watoto kwa huruma.
Ils briseront les arcs des jeunes hommes, ils seront sans pitié pour vos enfants; et vos fils, ils ne les épargneront point.
19 Babeli, johari ya falme, utukufu wa kiburi cha Wababeli, itaangushwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
Ainsi en sera-t-il de Babylone, que le roi des Chaldéens appelle glorieuse, comme de Sodome et de Gomorrhe, que Dieu a renversées.
20 Hautakaliwa na watu kamwe wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko, hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.
Elle ne sera plus jamais habitée, et l'on n'y rentrera plus durant de longues générations; et les Arabes ne la traverseront plus, et les pasteurs ne viendront plus s'y reposer.
21 Lakini viumbe wa jangwani watalala huko, mbweha watajaza nyumba zake, bundi wataishi humo nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.
Mais les bêtes fauves s'y reposeront, et ses maisons seront pleines de leurs cris; les dragons y feront leur séjour, et les démons y danseront;
22 Fisi watalia ndani ya ngome zake, mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari. Wakati wake umewadia, na siku zake hazitaongezwa.
Et les onocentaures y habiteront, et les hérissons feront leurs nids dans leurs demeures.