< Isaya 13 >

1 Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:
Oracle sur Babylone, révélé à Isaïe, fils d'Amots.
2 Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu, wapazieni sauti, wapungieni mkono waingie katika malango ya wenye heshima.
Sur une montagne nue levez un étendard; appelez-les à haute voix, faites des signes de la main, et qu'ils franchissent les portes des princes.
3 Nimewaamuru watakatifu wangu; nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu: wale wanaoshangilia ushindi wangu.
Moi, j'ai donné ordre à mes consacrés; j'ai appelé mes héros pour servir ma colère, ceux qui acclament avec joie ma majesté.
4 Sikilizeni kelele juu ya milima, kama ile ya umati mkubwa wa watu! Sikilizeni, makelele katikati ya falme, kama mataifa yanayokusanyika pamoja! Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.
On entend sur les montagnes une rumeur: on dirait le bruit d'un peuple nombreux; on entend un tumulte de royaumes, de nations rassemblées: C'est Yahweh des armées qui passe en revue ses troupes de guerre.
5 Wanakuja kutoka nchi za mbali sana, kutoka miisho ya mbingu, Bwana na silaha za ghadhabu yake, kuangamiza nchi yote.
Ils viennent d'un pays lointain, de l'extrémité du ciel, Yahweh et les instruments de son courroux, pour ravager toute la terre.
6 Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu, itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
Poussez des hurlements, car le jour de Yahweh est proche: il vient comme une dévastation du Tout-puissant.
7 Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
C'est pourquoi toute main sera défaillante, et tout cœur d'homme se fondra.
8 Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.
Ils trembleront, les transes et les douleurs les saisiront; ils se tordront comme une femme qui enfante; ils se regarderont les uns les autres avec stupeur; leurs visages seront comme la flamme.
9 Tazameni, siku ya Bwana inakuja, siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali, kuifanya nchi kuwa ukiwa na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.
Voici que le jour de Yahweh est venu, jour cruel, de fureur et d'ardente colère, pour réduire la terre en désert, et en exterminer les pécheurs.
10 Nyota za mbinguni na makundi ya nyota havitatoa mwanga wake. Jua linalochomoza litatiwa giza na mwezi hautatoa nuru yake.
Car les étoiles du ciel et leurs constellations ne font point briller leur lumière; le soleil s'est obscurci à son lever, et la lune ne répand plus sa clarté.
11 Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake, waovu kwa ajili ya dhambi zao. Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi, na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.
Je punirai le monde pour sa malice, et les méchants pour leur iniquité; je ferai cesser l'arrogance des superbes, et j'abaisserai l'orgueil des tyrans.
12 Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi, watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.
Je rendrai les hommes plus rares que l'or fin, plus rares que l'or d'Ophir.
13 Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke, nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika siku ya hasira yake iwakayo.
C'est pourquoi je ferai trembler les cieux, et la terre sera ébranlée de sa place, par la fureur de Yahweh des armées, au jour où s'allumera sa colère.
14 Kama swala awindwaye, kama kondoo wasio na mchungaji, kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.
Alors, comme une gazelle que l'on poursuit, comme un troupeau que personne ne rassemble, chacun se tournera vers son peuple, et s'enfuira dans son pays.
15 Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo, wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.
Tous ceux qu'on trouvera seront transpercés, tous ceux qu'on saisira tomberont par l'épée.
16 Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande mbele ya macho yao; nyumba zao zitatekwa na wake zao watatendwa jeuri.
Leurs petits enfants seront écrasés sous leurs yeux, leurs maisons pillées et leurs femmes violées.
17 Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao, ambao hawajali fedha wala hawafurahii dhahabu.
Voici que je fais lever contre eux les Mèdes, qui ne font point cas de l'argent, et ne convoitent pas l'or.
18 Mishale yao itawaangusha vijana, hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga wala hawataangalia watoto kwa huruma.
Leurs arcs écraseront les jeunes gens; ils ne feront point grâce au fruit des entrailles; leur œil n'aura pas pitié des enfants.
19 Babeli, johari ya falme, utukufu wa kiburi cha Wababeli, itaangushwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
Et Babylone, l'ornement des royaumes, la parure des fiers Chaldéens, sera comme Sodome et Gomorrhe que Dieu a détruites.
20 Hautakaliwa na watu kamwe wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko, hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.
Elle ne sera jamais plus peuplée, elle ne sera plus habitée dans le cours des âges; l'Arabe n'y dressera pas sa tente, et le berger n'y parquera pas ses troupeaux.
21 Lakini viumbe wa jangwani watalala huko, mbweha watajaza nyumba zake, bundi wataishi humo nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.
Les animaux du désert y feront leur gîte; les hiboux rempliront ses maisons; là habiteront les autruches, et le satyre y bondira.
22 Fisi watalia ndani ya ngome zake, mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari. Wakati wake umewadia, na siku zake hazitaongezwa.
Les chacals hurleront dans ses palais déserts, et les chiens sauvages dans ses maisons de plaisir. Son temps est proche, et ses jours ne seront pas prolongés.

< Isaya 13 >