< Isaya 12 >

1 Katika siku ile utasema: “Nitakusifu wewe, Ee Bwana. Ingawa ulinikasirikia, hasira yako imegeukia mbali nawe umenifariji.
וְאָֽמַרְתָּ בַּיּוֹם הַהוּא אוֹדְךָ יְהוָה כִּי אָנַפְתָּ בִּי יָשֹׁב אַפְּךָ וּֽתְנַחֲמֵֽנִי׃
2 Hakika Mungu ni wokovu wangu; nitamtumaini wala sitaogopa. Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu; amekuwa wokovu wangu.”
הִנֵּה אֵל יְשׁוּעָתִי אֶבְטַח וְלֹא אֶפְחָד כִּֽי־עָזִּי וְזִמְרָת יָהּ יְהוָה וַֽיְהִי־לִי לִֽישׁוּעָֽה׃
3 Kwa furaha mtachota maji kutoka visima vya wokovu.
וּשְׁאַבְתֶּם־מַיִם בְּשָׂשׂוֹן מִמַּעַיְנֵי הַיְשׁוּעָֽה׃
4 Katika siku hiyo mtasema: “Mshukuruni Bwana, mliitie jina lake; julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya, tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
וַאֲמַרְתֶּם בַּיּוֹם הַהוּא הוֹדוּ לַֽיהוָה קִרְאוּ בִשְׁמוֹ הוֹדִיעוּ בָֽעַמִּים עֲלִֽילֹתָיו הַזְכִּירוּ כִּי נִשְׂגָּב שְׁמֽוֹ׃
5 Mwimbieni Bwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu, hili na lijulikane duniani kote.
זַמְּרוּ יְהוָה כִּי גֵאוּת עָשָׂה מידעת מוּדַעַת זֹאת בְּכָל־הָאָֽרֶץ׃
6 Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni, kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”
צַהֲלִי וָרֹנִּי יוֹשֶׁבֶת צִיּוֹן כִּֽי־גָדוֹל בְּקִרְבֵּךְ קְדוֹשׁ יִשְׂרָאֵֽל׃

< Isaya 12 >