< Isaya 12 >

1 Katika siku ile utasema: “Nitakusifu wewe, Ee Bwana. Ingawa ulinikasirikia, hasira yako imegeukia mbali nawe umenifariji.
En ce jour-là, Israël, tu diras: Je vous bénis, Seigneur, parce que vous avez été irrité contre moi; puis vous avez détourné votre colère, et vous avez eu pitié de moi.
2 Hakika Mungu ni wokovu wangu; nitamtumaini wala sitaogopa. Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu; amekuwa wokovu wangu.”
Voici mon Dieu et mon Sauveur; je mettrai en lui ma confiance, et je serai sans crainte; parce que le Seigneur est ma gloire, il est ma louange, il est mon salut.
3 Kwa furaha mtachota maji kutoka visima vya wokovu.
Puisez avec joie l'eau des fontaines du salut.
4 Katika siku hiyo mtasema: “Mshukuruni Bwana, mliitie jina lake; julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya, tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
Et vous direz en ce jour: Chantez le Seigneur, célébrez son nom, annoncez sa gloire aux Gentils; souvenez-vous que son nom est glorifié.
5 Mwimbieni Bwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu, hili na lijulikane duniani kote.
Chantez le nom du Seigneur; car il a fait de grandes choses; publiez-les par toute la terre.
6 Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni, kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”
Tressaillez d'allégresse et réjouissez-vous, peuple de Sion; car au milieu de vous a été glorifié le Saint d'Israël.

< Isaya 12 >