< Isaya 12 >

1 Katika siku ile utasema: “Nitakusifu wewe, Ee Bwana. Ingawa ulinikasirikia, hasira yako imegeukia mbali nawe umenifariji.
And in that day thou shalt say: 'I will give thanks unto Thee, O LORD; for though Thou was angry with me, Thine anger is turned away, and Thou comfortest me.
2 Hakika Mungu ni wokovu wangu; nitamtumaini wala sitaogopa. Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu; amekuwa wokovu wangu.”
Behold, God is my salvation; I will trust, and will not be afraid; for GOD the LORD is my strength and song; and He is become my salvation.'
3 Kwa furaha mtachota maji kutoka visima vya wokovu.
Therefore with joy shall ye draw water out of the wells of salvation.
4 Katika siku hiyo mtasema: “Mshukuruni Bwana, mliitie jina lake; julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya, tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
And in that day shall ye say: 'Give thanks unto the LORD, proclaim His name, declare His doings among the peoples, make mention that His name is exalted.
5 Mwimbieni Bwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu, hili na lijulikane duniani kote.
Sing unto the LORD; for He hath done gloriously; this is made known in all the earth.
6 Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni, kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”
Cry aloud and shout, thou inhabitant of Zion, for great is the Holy One of Israel in the midst of thee.'

< Isaya 12 >