< Isaya 12 >

1 Katika siku ile utasema: “Nitakusifu wewe, Ee Bwana. Ingawa ulinikasirikia, hasira yako imegeukia mbali nawe umenifariji.
And thou shalt say in that day, O Lord, I will prayse thee: though thou wast angrie with me, thy wrath is turned away, and thou comfortest me.
2 Hakika Mungu ni wokovu wangu; nitamtumaini wala sitaogopa. Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu; amekuwa wokovu wangu.”
Beholde, God is my saluation: I will trust, and will not feare: for ye Lord God is my strength and song: he also is become my saluation.
3 Kwa furaha mtachota maji kutoka visima vya wokovu.
Therefore with ioy shall ye drawe waters out of the welles of saluation.
4 Katika siku hiyo mtasema: “Mshukuruni Bwana, mliitie jina lake; julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya, tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
And ye shall say in that day, Prayse the Lord: call vpon his Name: declare his workes among the people: make mention of them, for his Name is exalted.
5 Mwimbieni Bwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu, hili na lijulikane duniani kote.
Sing vnto the Lord, for he hath done excellent things: this is knowen in all the worlde.
6 Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni, kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”
Cry out, and shoute, O inhabitant of Zion: for great is ye holy one of Israel in the middes of thee.

< Isaya 12 >