< Isaya 11 >

1 Chipukizi litatokea kutoka shina la Yese, kutoka mizizi yake Tawi litazaa tunda.
İşay'ın kütüğünden yeni bir filiz çıkacak, Kökünden bir fidan meyve verecek.
2 Roho wa Bwana atakaa juu yake, Roho wa hekima na wa ufahamu, Roho wa shauri na wa uweza, Roho wa maarifa na wa kumcha Bwana
RAB'bin Ruhu, bilgelik ve anlayış ruhu, Öğüt ve güç ruhu, bilgi ve RAB korkusu ruhu Onun üzerinde olacak.
3 naye atafurahia kumcha Bwana. Hatahukumu kwa yale ayaonayo kwa macho yake, wala kuamua kwa yale ayasikiayo kwa masikio yake,
RAB korkusu hoşuna gidecek. Gözüyle gördüğüne göre yargılamayacak, Kulağıyla işittiğine göre karar vermeyecek.
4 bali kwa uadilifu atahukumu wahitaji, kwa haki ataamua wanyenyekevu wa dunia. Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, kwa pumzi ya midomo yake atawaua waovu.
Yoksulları adaletle yargılayacak, Yeryüzünde ezilenler için dürüstçe karar verecek. Dünyayı ağzının değneğiyle cezalandıracak, Kötüleri soluğuyla öldürecek.
5 Haki itakuwa mkanda wake na uaminifu utakuwa mshipi kiunoni mwake.
Davranışının temeli adalet ve sadakat olacak.
6 Mbwa mwitu ataishi pamoja na mwana-kondoo, naye chui atalala pamoja na mbuzi, ndama, mwana simba na ngʼombe wa mwaka mmoja watakaa pamoja, naye mtoto mdogo atawaongoza.
Onun döneminde kurtla kuzu bir arada yaşayacak, Parsla oğlak birlikte yatacak, Buzağı, genç aslan ve besili sığır yanyana duracak, Onları küçük bir çocuk güdecek.
7 Ngʼombe na dubu watalisha pamoja, watoto wao watalala pamoja, na simba atakula majani makavu kama maksai.
İnekle ayı birlikte otlayacak, Yavruları bir arada yatacak. Aslan sığır gibi saman yiyecek.
8 Mtoto mchanga atacheza karibu na shimo la nyoka, naye mtoto mdogo ataweka mkono wake kwenye kiota cha fira.
Emzikteki bebek kobra deliği üzerinde oynayacak, Sütten kesilmiş çocuk elini engerek kovuğuna sokacak.
9 Hawatadhuru wala kuharibu juu ya mlima wangu mtakatifu wote, kwa kuwa dunia itajawa na kumjua Bwana kama maji yajazavyo bahari.
Kutsal dağımın hiçbir yerinde Kimse zarar vermeyecek, yok etmeyecek. Çünkü sular denizi nasıl dolduruyorsa, Dünya da RAB'bin bilgisiyle dolacak.
10 Katika siku hiyo, Shina la Yese atasimama kama bendera kwa ajili ya mataifa. Mataifa yatakusanyika kwake, na mahali pake pa kupumzikia patakuwa utukufu.
O gün İşay'ın kökü ortaya çıkacak, Halklara sancak olacak, Uluslar ona yönelecek. Kaldığı yer görkemli olacak.
11 Katika siku hiyo Bwana atanyoosha mkono wake mara ya pili kurudisha mabaki ya watu wake waliosalia kutoka Ashuru, Misri, Pathrosi, Kushi, Elamu, Babeli, Hamathi na kutoka visiwa vya baharini.
O gün Rab, Asur'dan, Mısır, Patros, Kûş, Elam, Şinar, Hama ve deniz kıyılarından Halkının sağ kalanlarını kurtarmak için İkinci kez elini uzatacak.
12 Atainua bendera kwa mataifa na kuwakusanya Waisraeli walioko uhamishoni; atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika kutoka pembe nne za dunia.
Uluslar için sancak kaldıracak, Sürgün İsrailliler'i toplayacak, Dağılmış Yahudalılar'ı Dünyanın dört bucağından bir araya getirecek.
13 Wivu wa Efraimu utatoweka, na adui wa Yuda watakatiliwa mbali; Efraimu hatamwonea Yuda wivu, wala Yuda hatakuwa na uadui na Efraimu.
Efrayim halkının kıskançlığı yok olacak, Yahudalılar'ı sıkıştıranlar ortadan kalkacak. Efrayim Yahuda'yı kıskanmayacak, Yahuda Efrayim'i sıkıştırmayacak.
14 Watawashukia katika miteremko ya Wafilisti hadi upande wa magharibi, kwa pamoja watawateka watu nyara hadi upande wa mashariki. Watawapiga Edomu na Moabu, na Waamoni watatawaliwa nao.
Batıdaki Filistliler'e saldırıp Hep birlikte doğudakilerin her şeyini yağmalayacaklar. Edom ve Moav halklarının topraklarına el koyacak, Ammonlular'a boyun eğdirecekler.
15 Bwana atakausha ghuba ya bahari ya Misri; kwa upepo mkavu ataupeleka mkono wake juu ya Mto Frati. Ataugawanya katika vijito saba ili watu waweze kuuvuka wakiwa wamevaa viatu.
RAB Mısır'ın Süveyş Körfezi'ni tümüyle kurutacak. Elinin bir sallayışıyla estireceği kavurucu rüzgarla Fırat'ı süpürüp yedi dereye bölecek. Öyle ki, insanlar ırmak yatağından çarıkla geçebilsin.
16 Itakuwepo njia kuu kwa mabaki ya watu wake wale waliosalia kutoka Ashuru, kama ilivyokuwa kwa Israeli walipopanda kutoka Misri.
RAB'bin Asur'da sağ kalan halkı için Bir çıkış yolu olacak; Tıpkı Mısır'dan çıktıkları gün İsrailliler'in de bir çıkış yolu olduğu gibi.

< Isaya 11 >