< Isaya 11 >

1 Chipukizi litatokea kutoka shina la Yese, kutoka mizizi yake Tawi litazaa tunda.
从耶西的本必发一条; 从他根生的枝子必结果实。
2 Roho wa Bwana atakaa juu yake, Roho wa hekima na wa ufahamu, Roho wa shauri na wa uweza, Roho wa maarifa na wa kumcha Bwana
耶和华的灵必住在他身上, 就是使他有智慧和聪明的灵, 谋略和能力的灵, 知识和敬畏耶和华的灵。
3 naye atafurahia kumcha Bwana. Hatahukumu kwa yale ayaonayo kwa macho yake, wala kuamua kwa yale ayasikiayo kwa masikio yake,
他必以敬畏耶和华为乐; 行审判不凭眼见, 断是非也不凭耳闻;
4 bali kwa uadilifu atahukumu wahitaji, kwa haki ataamua wanyenyekevu wa dunia. Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, kwa pumzi ya midomo yake atawaua waovu.
却要以公义审判贫穷人, 以正直判断世上的谦卑人, 以口中的杖击打世界, 以嘴里的气杀戮恶人。
5 Haki itakuwa mkanda wake na uaminifu utakuwa mshipi kiunoni mwake.
公义必当他的腰带; 信实必当他胁下的带子。
6 Mbwa mwitu ataishi pamoja na mwana-kondoo, naye chui atalala pamoja na mbuzi, ndama, mwana simba na ngʼombe wa mwaka mmoja watakaa pamoja, naye mtoto mdogo atawaongoza.
豺狼必与绵羊羔同居, 豹子与山羊羔同卧; 少壮狮子与牛犊并肥畜同群; 小孩子要牵引它们。
7 Ngʼombe na dubu watalisha pamoja, watoto wao watalala pamoja, na simba atakula majani makavu kama maksai.
牛必与熊同食; 牛犊必与小熊同卧; 狮子必吃草,与牛一样。
8 Mtoto mchanga atacheza karibu na shimo la nyoka, naye mtoto mdogo ataweka mkono wake kwenye kiota cha fira.
吃奶的孩子必玩耍在虺蛇的洞口; 断奶的婴儿必按手在毒蛇的穴上。
9 Hawatadhuru wala kuharibu juu ya mlima wangu mtakatifu wote, kwa kuwa dunia itajawa na kumjua Bwana kama maji yajazavyo bahari.
在我圣山的遍处, 这一切都不伤人,不害物; 因为认识耶和华的知识要充满遍地, 好像水充满洋海一般。
10 Katika siku hiyo, Shina la Yese atasimama kama bendera kwa ajili ya mataifa. Mataifa yatakusanyika kwake, na mahali pake pa kupumzikia patakuwa utukufu.
到那日,耶西的根立作万民的大旗;外邦人必寻求他,他安息之所大有荣耀。
11 Katika siku hiyo Bwana atanyoosha mkono wake mara ya pili kurudisha mabaki ya watu wake waliosalia kutoka Ashuru, Misri, Pathrosi, Kushi, Elamu, Babeli, Hamathi na kutoka visiwa vya baharini.
当那日,主必二次伸手救回自己百姓中所余剩的,就是在亚述、埃及、巴忒罗、古实、以拦、示拿、哈马,并众海岛所剩下的。
12 Atainua bendera kwa mataifa na kuwakusanya Waisraeli walioko uhamishoni; atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika kutoka pembe nne za dunia.
他必向列国竖立大旗, 招回以色列被赶散的人, 又从地的四方聚集分散的犹大人。
13 Wivu wa Efraimu utatoweka, na adui wa Yuda watakatiliwa mbali; Efraimu hatamwonea Yuda wivu, wala Yuda hatakuwa na uadui na Efraimu.
以法莲的嫉妒就必消散; 扰害犹大的必被剪除。 以法莲必不嫉妒犹大, 犹大也不扰害以法莲。
14 Watawashukia katika miteremko ya Wafilisti hadi upande wa magharibi, kwa pamoja watawateka watu nyara hadi upande wa mashariki. Watawapiga Edomu na Moabu, na Waamoni watatawaliwa nao.
他们要向西飞, 扑在非利士人的肩头上, 一同掳掠东方人, 伸手按住以东和摩押; 亚扪人也必顺服他们。
15 Bwana atakausha ghuba ya bahari ya Misri; kwa upepo mkavu ataupeleka mkono wake juu ya Mto Frati. Ataugawanya katika vijito saba ili watu waweze kuuvuka wakiwa wamevaa viatu.
耶和华必使埃及海汊枯干, 抡手用暴热的风使大河分为七条, 令人过去不致湿脚。
16 Itakuwepo njia kuu kwa mabaki ya watu wake wale waliosalia kutoka Ashuru, kama ilivyokuwa kwa Israeli walipopanda kutoka Misri.
为主余剩的百姓, 就是从亚述剩下回来的, 必有一条大道, 如当日以色列从埃及地上来一样。

< Isaya 11 >