< Isaya 10 >

1 Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
¡Ay de los que decretan decretos injustos, y de los escritores que escriben decretos opresivos
2 kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
para privar a los necesitados de la justicia, y para despojar a los pobres de mi pueblo de sus derechos, para que las viudas sean su botín, y para que hagan del huérfano su presa!
3 Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
¿Qué harás en el día de la visitación y en la desolación que vendrá de lejos? ¿A quién huirás en busca de ayuda? ¿Dónde dejarás tus riquezas?
4 Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Sólo se inclinarán bajo los prisioneros, y caerá bajo los muertos. Por todo esto su ira no se desvía, pero su mano está extendida todavía.
5 “Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
¡Ay, Asirio, vara de mi ira, báculo en cuya mano está mi indignación!
6 Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
Lo enviaré contra una nación profana, y contra el pueblo que me enfurece le daré la orden de tomar el botín y de apoderarse de la presa, y de hollarlos como el lodo de las calles.
7 Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
Sin embargo, él no tiene esa intención, ni su corazón piensa así, sino que está en su corazón destruir, y cortar no pocas naciones.
8 Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
Porque dice: “¿No son todos mis príncipes reyes?
9 Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
¿No es Calno como Carchemish? ¿No es Hamat como Arpad? ¿No es Samaria como Damasco?”
10 Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
Como mi mano ha encontrado los reinos de los ídolos, cuyas imágenes grabadas superaban a las de Jerusalén y de Samaria,
11 je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
¿no haré, como he hecho con Samaria y sus ídolos, lo mismo con Jerusalén y sus ídolos?
12 Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
Por lo tanto, sucederá que cuando el Señor haya realizado toda su obra en el monte Sión y en Jerusalén, castigaré el fruto de la soberbia del corazón del rey de Asiria y la insolencia de su mirada arrogante.
13 Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
Porque él ha dicho: “Con la fuerza de mi mano lo he hecho, y con mi sabiduría, pues tengo entendimiento. He removido los límites de los pueblos, y he robado sus tesoros. Como un hombre valiente he derribado a sus gobernantes.
14 Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
Mi mano ha encontrado las riquezas de los pueblos como un nido, y como se recogen los huevos abandonados, he recogido toda la tierra. No hubo ninguno que moviera el ala, ni que abriera la boca, ni que piara”.
15 Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
¿Deberá el hacha jactarse del que corta con ella? ¿Acaso la sierra debe enaltecerse sobre el que sierra con ella? Como si una vara levantara al que la levanta, o como si un bastón levantara al que no es de madera.
16 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
Por eso el Señor, Yahvé de los Ejércitos, enviará entre sus gordos la delgadez; y bajo su gloria se encenderá un fuego como el fuego.
17 Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
La luz de Israel será como un fuego, y su Santo como una llama; y quemará y devorará sus espinas y sus cardos en un solo día.
18 Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
Consumirá la gloria de su bosque y de su campo fructífero, tanto el alma como el cuerpo. Será como cuando un abanderado desfallece.
19 Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
El remanente de los árboles de su bosque será escaso, de modo que un niño podría escribir su número.
20 Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Sucederá en ese día que el remanente de Israel y los que hayan escapado de la casa de Jacob no volverán a apoyarse en el que los golpeó, sino que se apoyarán en Yahvé, el Santo de Israel, en la verdad.
21 Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
Un remanente volverá, el remanente de Jacob, al Dios poderoso.
22 Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
Porque aunque tu pueblo, Israel, es como la arena del mar, sólo un remanente de él volverá. Se ha determinado una destrucción desbordante de justicia.
23 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
Porque el Señor, Yahvé de los Ejércitos, hará un final completo, y determinado, en toda la tierra.
24 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
Por eso el Señor, Yahvé de los Ejércitos, dice: “Pueblo mío que habitas en Sión, no tengas miedo del asirio, aunque te golpee con la vara y levante su bastón contra ti, como hizo Egipto.
25 Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
Todavía falta muy poco, y la indignación contra ustedes se cumplirá, y mi ira se dirigirá a su destrucción.”
26 Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
El Señor de los Ejércitos levantará un azote contra él, como en la matanza de Madián en la roca de Oreb. Su vara estará sobre el mar, y la levantará como lo hizo contra Egipto.
27 Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
Sucederá en ese día que su carga se apartará de tu hombro, y su yugo de tu cuello, y el yugo será destruido a causa del aceite de la unción.
28 Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
Ha llegado a Aiath. Ha pasado por Migrón. En Michmash guarda su equipaje.
29 Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
Han atravesado el paso. Se han alojado en Geba. Ramá tiembla. Gabaa de Saúl ha huido.
30 Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
¡Grita con tu voz, hija de Galim! ¡Escucha, Laishah! ¡Pobre Anatot!
31 Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
Madmena es una fugitiva. Los habitantes de Gebim huyen para ponerse a salvo.
32 Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
Hoy mismo se detendrá en Nob. Se estrechará en el monte de la hija de Sión, en la colina de Jerusalén.
33 Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
He aquí que el Señor, Yahvé de los Ejércitos, cortará las ramas con terror. Los altos serán cortados, y los altivos serán abatidos.
34 Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.
Élcortará con hierro los matorrales del bosque, y el Líbano caerá por el Poderoso.

< Isaya 10 >