< Isaya 10 >
1 Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
Malheur à ceux qui font des ordonnances d'iniquité, et qui dictent l'oppression qu'on leur a dictée.
2 kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
Pour enlever aux chétifs de leur droit, et pour ravir le droit des affligés de mon peuple, afin d'avoir les veuves pour leur butin, et de piller les orphelins.
3 Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
Et que ferez-vous au jour de la visitation, et de la ruine éclatante qui viendra de loin? vers qui recourrez-vous pour avoir du secours, et où laisserez-vous votre gloire?
4 Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Sans qu'aucun soit courbé sous les prisonniers, ils tomberont même sous ceux qui auront été tués. Malgré tout cela il ne fera point cesser sa colère, mais sa main sera encore étendue.
5 “Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
Malheur à Assur, la verge de ma colère; quoique le bâton qui est en leur main [soit] mon indignation.
6 Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
Je l'enverrai contre la nation hypocrite, et je le dépêcherai contre le peuple de ma fureur, afin qu'il fasse un grand butin, et un grand pillage, et qu'il le foule comme la boue des rues.
7 Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
Mais il ne l'estimera pas ainsi, et son cœur ne le pensera pas ainsi; mais [il aura] en son cœur de détruire et d'exterminer beaucoup de nations.
8 Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
Car il dira; mes Princes ne sont-ils pas autant de Rois?
9 Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
Calno, n'est-elle pas comme Carchémis? Hamath, n'est-elle pas comme Arpad? et Samarie, n'est-elle pas comme Damas?
10 Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
Ainsi que ma main a soumis les Royaumes [qui avaient] des idoles, et desquels les images taillées [valaient plus] que [celles] de Jérusalem et de Samarie;
11 je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
Ne ferai-je pas aussi à Jérusalem et à ses dieux, comme j'ai fait à Samarie et à ses idoles?
12 Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
Mais il arrivera que quand le Seigneur aura achevé toute son œuvre dans la montagne de Sion et à Jérusalem, j'examinerai le fruit de la grandeur du cœur du Roi d'Assyrie, et la gloire de la fierté de ses yeux.
13 Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
Parce qu'il aura dit; je l'ai fait par la force de ma main, et par ma sagesse, car je suis intelligent; j'ai ôté les bornes des peuples, et j'ai pillé ce qu'ils avaient de plus précieux, et comme puissant j'ai fait descendre ceux qui étaient assis.
14 Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
Et ma main a trouvé comme un nid les richesses des peuples; et ainsi qu'on rassemble les œufs délaissés, ainsi ai-je rassemblé toute la terre, et il n'y a eu personne qui ait remué l'aile, ou qui ait ouvert le bec, ou qui ait grommelé.
15 Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
La cognée se glorifiera-t-elle contre celui qui en coupe? ou la scie se magnifiera-t-elle contre celui qui la remue? comme si la verge se remuait contre ceux qui la lèvent en haut, et que le bâton s'élevât, [comme] s'il n'était pas du bois.
16 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
C'est pourquoi le Seigneur, l'Eternel des armées enverra la maigreur sur ses hommes gras, et par le dessous de sa gloire il allumera un embrasement, tel que l'embrasement d'un feu.
17 Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
Car la lumière d'Israël sera un feu, et son Saint sera une flamme, qui embrasera et consumera ses épines et ses ronces tout en un jour.
18 Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
Et il consumera la gloire de sa forêt, et de son Carmel, depuis l'âme jusqu'à la chair; et il en sera comme quand celui qui porte l'étendart est défait.
19 Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
Et le reste des arbres de sa forêt seront aisés à compter, tellement qu'un enfant les mettrait bien en écrit.
20 Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Et il arrivera en ce jour-là que le résidu d'Israël, et ceux qui seront réchappés de la maison de Jacob, ne s'appuieront plus sur celui qui les frappait, mais ils s'appuieront en vérité sur l'Eternel, le Saint d'Israël.
21 Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
Le résidu sera converti, le résidu, [dis-je], de Jacob [sera converti] au [Dieu] Fort et puissant.
22 Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
Car, ô Israël! quand ton peuple serait comme le sablon de la mer, un résidu en sera converti, [mais] la consomption déterminée fera déborder la justice.
23 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
Car le Seigneur l'Eternel des armées s'en va faire une consomption, même déterminée, au milieu de toute la terre.
24 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
C'est pourquoi ainsi a dit le Seigneur l'Eternel des armées; mon peuple qui habites dans Sion, ne crains point le Roi d'Assyrie; il te frappera de la verge, et il lèvera son bâton sur toi à la manière d'Egypte.
25 Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
Mais encore un peu de temps, un peu de temps, et [mon] indignation sera consommée, et ma colère sera à leur destruction.
26 Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
Et l'Eternel des armées lèvera sur lui un fouet, [qui sera] comme la plaie de Madian au rocher d'Horeb; et [comme] son bâton sur la mer, lequel il élèvera aussi comme contre les Egyptiens.
27 Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
Et il arrivera en ce jour-là, que son fardeau sera ôté de dessus ton épaule, et son joug de dessus ton cou; et le joug sera rompu à cause de l'onction.
28 Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
Il est venu à Hajath, il est passé à Migron, et il a mis son bagage à Michmas.
29 Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
Ils ont passé le gué; ils ont fait leur gîte à Guébah, Rama s'est effrayée, Guibha-Saül s'en est fuie.
30 Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
Fille de Gallim, élève ta voix, pauvre Hanathoth, fais-toi ouïr vers Laïs.
31 Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
Madména s'est écartée, les habitants de Guébim s'en sont fuis en foule.
32 Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
Encore un jour, il s'arrêtera à Nob; il lèvera sa main [contre] la montagne de la fille de Sion, [contre] le coteau de Jérusalem.
33 Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
Voici, le Seigneur, l'Eternel des armées ébranchera les rameaux avec force, et ceux qui sont les plus haut élevés, seront coupés; et les haut montés seront abaissés.
34 Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.
Et il taillera avec le fer les lieux les plus épais de la forêt, et le Liban tombera avec impétuosité.