< Isaya 10 >

1 Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
Malheur à ceux qui écrivent l'iniquité! car en écrivant ainsi, c'est l'iniquité qu'ils gravent.
2 kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
Ils écartent du pauvre la justice, ils arrachent tout moyen de défense aux indigents de mon peuple, afin que la veuve soit pour eux un butin, l'orphelin une proie.
3 Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
Et que feront-ils au jour de la visite du Seigneur? car la tribulation viendra sur vous de loin. Vers qui vous réfugierez-vous pour avoir du secours? Et où cacherez-vous votre gloire,
4 Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Pour n'être point entraînés en captivité? Sur vous tous s'est tournée la colère du Seigneur, et sa main est encore levée.
5 “Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
Malheur aux Assyriens! la verge de mon courroux, ma colère est dans leurs mains.
6 Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
J'enverrai ma colère contre une nation inique, et je commanderai à mon peuple de recueillir du butin et des dépouilles, de fouler aux pieds les villes et de les réduire en poussière.
7 Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
Mais lui, telle n'est point sa pensée, tel n'est point le sentiment de son âme. Il mettra son orgueil à exterminer de nombreuses nations.
8 Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
Et si elles lui disent: Toi seul es roi;
9 Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
Il répondra: En effet, n'ai-je point pris la contrée au-dessus de Babylone, et Chalane où une tour a été construite? N'ai-je point pris l'Arabie, et Damas, et Samarie?
10 Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
Comme je les ai prises, ainsi je prendrai tous les royaumes. Lamentez- vous, statues de Jérusalem et de Samarie!
11 je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
Comme j'ai traité Samarie et les dieux fabriqués de ses mains, je traiterai Jérusalem et ses idoles.
12 Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
Puis voici ce qui arrivera: quand le Seigneur aura achevé d'accomplir ce qu'il veut faire en la montagne de Sion et à Jérusalem, je visiterai ce cœur superbe, ce roi des Assyriens, et la gloire altière de ses yeux.
13 Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
Car il a dit: J'agirai dans ma force; et dans la sagesse de mon intelligence j'effacerai les bornes des nations, et je les dépouillerai de leur puissance.
14 Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
Et j'ébranlerai les villes habitées; et la terre entière, je la prendrai comme un nid dans ma main; et je l'enlèverai comme des œufs abandonnés; car nul ne peut m'échapper ou me contredire.
15 Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
Mais la cognée peut-elle se glorifier sans celui qui s'en sert pour abattre? La scie peut-elle s'enorgueillir sans celui qui la tire? Il faut bien que quelqu'un lève la verge ou le bâton; mais non.
16 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
Le Seigneur des armées enverra contre ton honneur le déshonneur, et contre ta gloire il allumera un feu ardent.
17 Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
Et la lumière d'Israël sera cette flamme; elle le sanctifiera avec un feu ardent, et dévorera la forêt comme une herbe sèche.
18 Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
En ce jour s'évanouiront montagnes, collines et forêts, et la lumière d'Israël dévorera tout, depuis l'âme jusqu'aux chairs. Et celui qui fuira sera comme un homme qui fuit une flamme ardente;
19 Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
Et ceux qui resteront seront en petit nombre, et un petit enfant pourra les compter.
20 Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Et en ce jour voici ce qui arrivera: ce qui restera d'Israël, et ceux de Jacob qui auront été sauvés n'auront plus foi en ceux qui leur auront nui; mais ils se confieront en vérité à Dieu, au Saint d'Israël.
21 Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
Et ce qui restera de Jacob se confiera au Dieu tout-puissant.
22 Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
Et quand le peuple d'Israël serait aussi nombreux que le sable de la mer, un reste en sera seul sauvé.
23 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
Parole abrégée et accomplie avec justice; car cette parole abrégée, le Seigneur l'étendra à toute la terre.
24 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
A cause de cela, voici ce que dit le Seigneur des armées: Ne crains pas, ô mon peuple; habitants de Sion, ne craignez pas l'Assyrien; il te frappera avec une verge; car j'amènerai sur toi cette plaie, pour que tu y reconnaisses la voie d'Égypte.
25 Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
Encore un peu de temps, et ma colère s'apaisera; mais alors mon courroux se tournera contre les conseils de tes ennemis.
26 Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
Et le Seigneur suscitera contre eux une plaie semblable à celle de Madian dans le lieu de l'affliction; et son courroux éclatera comme autrefois contre l'Égypte sur le chemin de la mer Rouge.
27 Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
Et en ce jour voici ce qui arrivera: ton joug sera ôté de ton épaule, et tu seras délivré de ta crainte, et le joug qui pesait sur tes épaules sera réduit en poudre.
28 Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
Il marchera d'abord sur la ville d'Aggaï, passera par Maggédo et déposera à Machma ses appareils de guerre.
29 Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
Puis il traversera la vallée et entrera dans Aggaï; la terreur saisira Rama, ville de Saul.
30 Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
La fille de Gallim prendra la fuite; on l'apprendra à Lasa, on l'apprendra à Anathoth.
31 Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
Et la stupeur a frappé Madebina, et les habitants de Gibbeïr.
32 Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
Pour vous, consolez-vous aujourd'hui et restez fermes dans la voie; ô vous, collines de Jérusalem, consolez la montagne et Sion, ma fille.
33 Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
Voilà que le maître, le Seigneur des armées, va de sa puissance confondre ces glorieux; et les grands seront brisés avec leur orgueil; et les superbes seront humiliés,
34 Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.
Et les superbes périront car le glaive; et le Liban tombera avec ses cîmes.

< Isaya 10 >