< Isaya 10 >

1 Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
Wo to them that maken wickid lawis, and thei writynge han wryte vnriytfulnesse, for to oppresse pore men in doom,
2 kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
and to do violence to the cause of meke men of my puple; that widewis schulen be the prey of them, and that thei schulden rauysche fadirles children.
3 Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
What schulen ye do in the dai of visitacioun, and of wretchidnesse comynge fro fer? To whos help schulen ye fle? and where schulen ye leeue youre glorie,
4 Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
that ye be not bowid doun vndur boond, and falle not doun with slayn men? On alle these thingis his strong veniaunce is not turned awei, but yit his hond is stretchid forth.
5 “Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
Wo to Assur, he is the yerde and staf of my strong veniaunce; myn indignacioun is in the hond of them.
6 Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
Y schal send hym to a fals folk, and Y schal comaunde to hym ayens the puple of my strong veniaunce; that he take awei the spuylis, and departe prey, and that he sette that puple in to defouling, as the fen of stretis.
7 Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
Forsothe he schal not deme so, and his herte schal not gesse so, but his herte schal be for to al to-breke, and to the sleynge of many folkis.
8 Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
For he schal seie, Whether my princes ben not kyngis to gidere?
9 Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
Whether not as Carcamys, so Calanno; and as Arphat, so Emath? whether not as Damask, so Samarie?
10 Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
As myn hond foond the rewmes of idol, so and the symylacris of hem of Jerusalem and of Samarie.
11 je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
Whether not as Y dide to Samarie, and to the idols therof, so Y schal do to Jerusalem, and to the simylacris therof?
12 Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
And it schal be, whanne the Lord hath fillid alle hise werkis in the hil of Syon and in Jerusalem, Y schal visite on the fruit of the greet doynge herte of the kyng of Assur, and on the glorie of the hiynesse of hise iyen.
13 Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
For he seide, Y haue do in the strengthe of myn honde, and Y haue understonde in my wisdom; and Y haue take awei the endis of peplis, and Y haue robbid the princes of them, and Y as a myyti man haue drawun doun them that saten an hiy.
14 Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
And myn hond foond the strengthe of puplis as a nest, and as eirun ben gaderid togidere that ben forsakun, so Y gaderid togidere al erthe; and noon was that mouyde a fethere, and openyde the mouth, and grutchide.
15 Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
Whether an ax schal haue glorie ayens hym that kittith with it? ether a sawe schal be enhaunsid ayens hym of whom it is drawun? as if a yerde is reisid ayens hym that reisith it, and a staf is enhaunsid, which sotheli is a tre.
16 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
For this thing the lordli gouernour, Lord of oostis, schal sende thinnesse in the fatte men of hym, and his glorie kyndlid vndur schal brenne as `the brenning of fier.
17 Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
And the liyt of Israel schal be in fier, and the hooli of it in flawme; and the thorn of him and brere schal be kyndlid and deuourid in o dai.
18 Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
And the glorie of his forest and of his Carmele schal be wastid, fro the soule `til to fleisch; and he schal be fleynge awei for drede.
19 Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
And the relifs of the tree of his forest schulen be noumbrid for fewnesse, and a child schal write hem.
20 Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
And it schal be in that dai, the remenaunt of Israel, and thei that fledden of the house of Jacob, schal not adde for to triste on hym that smytith hem; but it schal triste on the hooli Lord of Israel, in treuthe.
21 Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
The relifs, Y seie, the relifs of Jacob, schulen be conuertid to the stronge Lord.
22 Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
Forwhi, Israel, if thi puple is as the grauel of the see, the relifs schulen be turned therof; an endyng maad schort schal make riytfulnesse to be plenteuouse.
23 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
For whi the Lord God of oostis schal make an endyng and a breggyng in the myddis of al erthe.
24 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
For this thing the Lord God of oostis seith these thingis, My puple, the dwellere of Sion, nyle thou drede of Assur, for he schal smite thee in a yerde, and he schal reise his staf on thee in the weie of Egipt.
25 Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
Forwhi yit a litil, and a litil, and myn indignacioun and my strong veniaunce schal be endid on the greet trespas of hem.
26 Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
And the Lord of oostis schal reise a scourge on hym bi the veniaunce of Madian in the stoon of Oreb, and bi his yerde on the see; and he schal reise that yerde in the wei of Egipt.
27 Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
And it schal be in that dai, his birthun schal be takun awei fro thi schuldre, and his yok fro thi necke; and the yok schal wexe rotun fro the face of oile.
28 Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
He schal come in to Aioth, he schal passe in to Magron, at Magynas he schal bitake his vessels to kepyng.
29 Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
Thei passiden swiftli, Gabaa is oure seete, Rama was astonyed, Gabaa of Saul fled.
30 Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
Thou douytir of Gallym, weile with thi vois; thou Laisa, perseyue, thou pore Anatot.
31 Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
Medemena passide; the dwelleris of Gabyn fledden; be ye coumfortid.
32 Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
Yit it is dai, that me stonde in Nobe; he schal dryue his hond on the hil of the douyter of Syon, on the litil hil of Jerusalem.
33 Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
Lo! the lordli gouernour, the Lord of oostis, schal breke a potel in drede, and hiy men of stature schulen be kit doun.
34 Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.
And proude men schulen be maade low, and the thicke thingis of the forest schulen be distried bi irun; and the Liban with hiy thingis schal falle doun.

< Isaya 10 >