< Isaya 10 >
1 Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
Woe to them that make unrighteous decrees, That write oppressive decisions,
2 kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
To turn away the needy from judgment, And rob the poor of my people of their right; That the widows may become their prey, And that they may plunder the orphans.
3 Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
What will ye do in the day of visitation, And in the desolation which cometh from afar? To whom will ye flee for help, And where will ye leave your glory?
4 Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Forsaken by me, they shall sink down among the prisoners, And fall among the slain. For all this his anger is not turned away, But his hand is stretched out still.
5 “Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
Woe to the Assyrian, the rod of mine anger, The staff in whose hands is the instrument of my indignation!
6 Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
Against an impious nation I will send him, And against a people under my wrath I will give him a charge To gather the spoil, and seize the prey, And to trample them under foot like the mire of the streets.
7 Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
But he doth not so purpose, And his heart doth not so intend; But to destroy is in his heart, And to cut off a multitude of nations.
8 Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
For he saith, “Are not my princes altogether kings?
9 Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
Is not Calno as Carchemish? Is not Hamath as Arpad? Is not Samaria as Damascus?
10 Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
As my hand hath seized the kingdoms of the idols, Whose graven images were more numerous than those of Jerusalem and Samaria,
11 je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
Behold! as I have done to Samaria and her idols, So will I do to Jerusalem and her images.”
12 Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
But when the Lord hath accomplished his whole work upon Mount Zion and Jerusalem, Then will he punish the fruit of the proud heart of the king of Assyria, And the arrogance of his lofty eyes.
13 Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
For he hath said: “By the strength of my hand I have done it, And by my wisdom; for I am wise; I have removed the bounds of nations, I have plundered their treasures; As a hero have I brought down them that sat upon thrones.
14 Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
The riches of the nations hath my hand seized, as a nest; As one gathereth eggs that have been left, So have I gathered the whole world. And there was none that moved the wing, Or that opened the beak, or that chirped.”
15 Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
Shall the axe boast itself against him that heweth with it? Or shall the saw magnify itself against him that moveth it? As if the rod should wield him that lifteth it! As if the staff should lift up him that is not wood!
16 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
Wherefore the Lord, the Lord of hosts, shall send upon his fat ones leanness, And under his glory shall he kindle a burning, like the burning of a fire.
17 Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
The light of Israel shall be a fire, And his Holy One a flame, Which shall burn and devour his thorns and briers in one day.
18 Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
The glory of his forest and of his fruitful field From the spirit even to the flesh shall he consume; It shall be with them as when a sick man fainteth.
19 Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
The remaining trees of the forest shall be few, So that a child may write them down.
20 Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
In that day shall the remnant of Israel, and they that have escaped of the house of Jacob, no more lean upon him that smote them; They shall lean upon Jehovah, the Holy One of Israel, in truth.
21 Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
The remnant shall return, the remnant of Jacob, to the mighty Potentate;
22 Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
For though thy people, O Israel, be as the sand of the sea, Only a remnant of them shall return. The devastation is decreed; It shall overflow with righteousness.
23 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
For devastation and punishment doth the Lord, Jehovah of hosts, execute in the midst of the whole land,
24 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
Yet thus saith the Lord, Jehovah of hosts: Fear not, O my people, that dwellest in Zion, because of the Assyrian! With his rod indeed shall he smite thee, And lift up his staff against thee in the manner of Egypt;
25 Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
But yet a very little while, and my indignation shall have past, And my anger shall destroy them.
26 Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
Jehovah of hosts shall raise up against him a scourge, As he smote Midian at the rock of Horeb, And as he lifted up the rod against the sea; Yea, he shall lift it up, as in Egypt.
27 Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
In that day shall his burden be removed from thy shoulder, And his yoke from thy neck; Yea, thy yoke shall be broken, as that of a fat steer.
28 Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
He is come to Aiath; he passeth through Migron; In Michmash he leaveth his baggage;
29 Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
They pass the strait; At Geba they make their night-quarters; Ramah trembleth; Gibeah of Saul fleeth.
30 Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
Cry aloud, O daughter of Gallim! Hear, O Laish! Alas, poor Anathoth!
31 Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
Madmenah hasteth away; The inhabitants of Gebim take to flight.
32 Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
Yet one day shall he rest at Nob, Then shall he shake his hand against the mount of the daughter of Zion, The hill of Jerusalem.
33 Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
But behold! the Lord, Jehovah of hosts, shall lop the branches with fearful force, And the high of stature shall be cut down, And the lofty shall be brought low.
34 Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.
He shall hew the thickets of the forest with iron, And Lebanon shall fall by a mighty hand.