< Isaya 10 >

1 Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
Tragedy is coming to those who pass evil decrees and who write laws to harm people.
2 kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
They pervert the legal rights of the needy, and rob justice from the poor of my people. They steal from widows and cheat orphans.
3 Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
What are you going to do on the day you're punished, when disaster falls on you from far away? Who are you going to run to so you can get help? Where are you going to leave all your wealth?
4 Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
All you'll be able to do is to bow down as prisoners, or lie among the dead! In all of this he is still angry and his hand is still raised.
5 “Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
Tragedy is coming to the Assyrians, even though the rod they use represents my anger and the stick they hold in their hands represents my fury!
6 Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
I am sending the Assyrians against a nation that has given up on its God, against a people that make me angry. I order the Assyrians to loot them, to take their possessions, and to trample them down like mud in the street.
7 Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
But this isn't what is behind the thinking of the king of Assyria. This isn't the plan he has in mind. What he wants to do is to destroy and eliminate many nations.
8 Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
He says: “All my commanders are kings!
9 Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
We conquered Calno like we did Carchemish; Hamath like Arpad; Samaria like Damascus.
10 Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
I was the one who conquered these kingdoms along with the idols of their gods. These kingdoms had images of their gods that were better than those of Jerusalem and Samaria.
11 je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
Why shouldn't I do to Jerusalem and her idols just what I did to Samaria and her idols?”
12 Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
Once the Lord has finished all his work against Mount Zion and Jerusalem, he will punish the king of Assyria for his terrible arrogance and for the conceited look in his eyes.
13 Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
For the king of Assyria says: “I have done this in my own strength. It was through my wisdom, because I'm clever. I have wiped out the boundaries of nations and looted their treasures. Like a bull I knocked their rulers off their thrones.
14 Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
Like robbing a bird's nest, I took the wealth of the nations. Like collecting abandoned eggs, I collected the whole the earth. There wasn't a fluttering wing or an open beak, not even a chirp!”
15 Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
Does an ax say it's more important than the person swinging it? Does a saw boast that it's greater than the person sawing with it? It would be as if a rod waved the person holding it, or a walking stick lifted up a person—who certainly wasn't wood!
16 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
So the Lord, the Lord Almighty, will send a disease on the king of Assyria's strong warriors that will make them waste away; a flaming fire will be set under everything he's so proud of.
17 Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
Israel's light will become a fire, and his Holy One will become a flame. It will burn up his thorns and brambles in just one day.
18 Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
It will totally destroy its splendid forests and orchards. Assyria will waste away, staggering off like someone sick.
19 Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
The trees left in its forests will be so few that a child could count them.
20 Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
At that time those who are left in Israel and the survivors of the house of Jacob will no longer trust in those who turn on them, but they will truly trust in the Lord, the Holy One of Israel.
21 Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
A remnant will return, a remnant of Jacob will come back to the Mighty God.
22 Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
Israel, even though your people are as numerous as sand on the seashore, only a remnant will return. The Lord has rightly decided to destroy his people.
23 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
The Lord God Almighty has rightly decided to bring destruction throughout the whole country.
24 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
So this is what the Lord, the Lord Almighty, says, My people living in Zion, don't be afraid of the Assyrians who beat you with rods and hit you with clubs, just like the Egyptians did.
25 Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
Very shortly I will stop being angry with you. Then I will turn my anger on them and I will destroy them.
26 Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
The Lord Almighty will lash them with a whip, just as he did when he attacked the Midianites at the rock of Oreb. He will hold up his rod over the sea, just as he did in Egypt.
27 Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
At that time he will remove the burden from your shoulders and the yoke from your neck. The yoke will be broken because of the anointing with oil.
28 Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
The Assyrians came to Aiath, passed through Migron, and stored their supplies at Michmash.
29 Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
They cross the pass, saying, “We'll stay overnight at Geba.” The people of Ramah tremble in fear; the inhabitants of Gibeah of Saul run away.
30 Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
Shout out a warning, people of Gallim! Pay attention, those living in Laishah! You poor people of Anathoth!
31 Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
The people of Madmenah, are all running away. The inhabitants of Gebim are looking for somewhere safe.
32 Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
Today the invaders stop at Nob, shaking their fists at the mountain of the Daughter of Zion, at the hill of Jerusalem.
33 Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
Look how the Lord Almighty is going to chop off the branches with great force. The tall trees will be cut down, the proud trees will be brought crashing down.
34 Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.
He will cut down the thick forest with an ax, and Lebanon will fall at the hand of the Mighty One.

< Isaya 10 >