< Isaya 1 >
1 Maono kuhusu Yuda na Yerusalemu ambayo Isaya mwana wa Amozi aliyaona wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.
La visión de Isaías, hijo de Amoz, que vio sobre Judá y Jerusalén, en los días de Uzías, Jotam, Acaz y Ezequías, reyes de Judá.
2 Sikieni, enyi mbingu! Sikilizeni, enyi dunia! Kwa maana Bwana amesema: “Nimewalisha watoto na kuwalea, lakini wameniasi mimi.
Escucha, oh cielos, y tú, oh tierra, a la palabra que el Señor ha dicho: He cuidado de mis hijos hasta que se han hecho hombres, pero sus corazones se han apartado de mí.
3 Ngʼombe anamjua bwana wake, naye punda anajua hori la mmiliki wake, lakini Israeli hajui, watu wangu hawaelewi.”
Incluso el buey tiene conocimiento de su dueño, y el asno del lugar donde su amo pone su comida; pero Israel no tiene conocimiento, mi pueblo no entiende.
4 Lo! Taifa lenye dhambi, watu waliolemewa na uovu, uzao wa watenda mabaya, watoto waliozoelea upotovu! Wamemwacha Bwana, Wamemkataa kwa dharau yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli na kumgeuzia kisogo.
Oh nación llena de pecado, un pueblo cargado de crimen, una generación de malhechores, hijos de falso corazón! se han ido del Señor, no tienen respeto por el Santo de Israel, sus corazones se apartaron de él.
5 Kwa nini mzidi kupigwa? Kwa nini kudumu katika uasi? Kichwa chako chote kimejeruhiwa, moyo wako wote ni mgonjwa.
¿Por qué tendrás más y más castigo? ¿Por qué seguir en tus malos caminos? Toda cabeza está enferma y todo corazón desfallecido.
6 Kutoka wayo wako wa mguu hadi kwenye utosi wa kichwa chako hakuna uzima: ni majeraha matupu na makovu na vidonda vitokavyo damu, havikusafishwa au kufungwa wala kulainishwa kwa mafuta.
El cuerpo, de pies a cabeza, está todo enfermo; Es una masa de heridas abiertas, marcas de golpes y heridas; el flujo de sangre no se ha detenido y no se ha puesto aceite en las heridas.
7 Nchi yenu imekuwa ukiwa, miji yenu imeteketezwa kwa moto; nchi yenu imeachwa tupu na wageni mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile imepinduliwa na wageni.
Tu país se ha convertido en un desperdicio; tus pueblos son quemados con fuego; En cuanto a tu tierra, se volcó ante tus ojos, fue desechada y vencida por hombres de tierras extrañas.
8 Binti Sayuni ameachwa kama kipenu katika shamba la mizabibu, kama kibanda katika shamba la matikitimaji, kama mji uliohusuriwa.
Y la hija de Sión se ha convertido en una tienda de campaña en un jardín de viñas, como la casa de un vigilante en un campo de frutas, como una ciudad cerrada por ejércitos.
9 Kama Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asingelituachia walionusurika, tungelikuwa kama Sodoma, tungelifanana na Gomora.
Si el Señor de los ejércitos no hubiera mantenido a salvo a algunos de nosotros, habríamos sido como Sodoma, y el destino de Gomorra habría sido el nuestro.
10 Sikieni neno la Bwana, ninyi watawala wa Sodoma; sikilizeni sheria ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora!
Escuchen la palabra del Señor, gobernantes de Sodoma; Que sus corazones se vuelvan a la ley de nuestro Dios, pueblo de Gomorra.
11 Bwana anasema, “Wingi wa sadaka zenu, ni kitu gani kwangu? Ninazo sadaka za kuteketezwa nyingi kupita kiasi, za kondoo dume na mafuta ya wanyama walionona. Sipendezwi na damu za mafahali wala za wana-kondoo na mbuzi.
¿Para qué me sirve el número de las ofrendas que me dan? dice el Señor sus ofrendas quemadas de ovejas, y las mejores partes del ganado gordo, estoy harto de ellas; No me complace de la sangre de los bueyes, ni de los corderos, ni de los chivos.
12 Mnapokuja kujihudhurisha mbele zangu, ni nani aliyewataka ninyi mfanye hivyo, huku kuzikanyaga nyua zangu?
¿A cuando vienen delante de mí, Quien demanda esto de ustedes, pisoteando mis atrios?
13 Acheni kuniletea sadaka zisizokuwa na maana! Uvumba wenu ni chukizo kwangu. Miandamo ya Mwezi, Sabato na makusanyiko ya ibada: siwezi kuvumilia makusanyiko yenu maovu.
No me traigan falsas ofrendas; el incienso para mi es una abominación. Luna nueva y día de reposo, el convocar asambleas, no soporto la iniquidad de sus asambleas solemnes.
14 Sikukuu zenu za Miandamo ya Mwezi, na sikukuu zenu zilizoamriwa: moyo wangu unazichukia. Zimekuwa mzigo kwangu, nimechoka kuzivumilia.
Sus nuevas lunas y sus fiestas regulares, son un dolor para mi alma, son un peso en mi espíritu; Estoy cansado de esa carga.
15 Mnaponyoosha mikono yenu katika maombi, nitaficha macho yangu nisiwaone; hata mkiomba maombi mengi sitasikiliza. Mikono yenu imejaa damu;
Y cuando tengan sus manos extendidas hacia mí, mis ojos se apartarán de ustedes; aunque sigan haciendo oraciones, no escucharé; sus manos están llenas de sangre.
16 jiosheni na mkajitakase. Yaondoeni matendo yenu maovu mbele zangu! Acheni kutenda mabaya,
Se lavan, se limpian; aparten el mal de sus obras delante de mis ojos; Sea el fin del pecado.
17 jifunzeni kutenda mema! Tafuteni haki, watieni moyo walioonewa. Teteeni shauri la yatima, wateteeni wajane.
Aprendan hacer el bien; busquen la justicia, mantén al margen a los crueles, defiende al niño que no tiene padre, cuida la causa de la viuda.
18 “Njooni basi tuhojiane,” asema Bwana. “Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu, zitakuwa nyeupe kama theluji; ingawa ni nyekundu sana kama damu, zitakuwa nyeupe kama sufu.
Vengan, y discutamos juntos, dice el Señor: aunque sus pecados sean como la grana, yo los dejaré blancos como la nieve; Aunque sean rojos como él carmesí, quedarán blancos como lana.
19 Kama mkikubali na kutii, mtakula mema ya nchi,
Si escuchan mi palabra y la cumplen, las cosas buenas de la tierra serán suyas.
20 lakini kama mkikataa na kuasi, mtaangamizwa kwa upanga.” Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena.
Pero si sus corazones se vuelven contra mí, les enviaré la destrucción por la espada; así ha dicho el Señor.
21 Tazama jinsi mji uliokuwa mwaminifu umekuwa kahaba! Mwanzoni ulikuwa umejaa unyofu, haki ilikuwa inakaa ndani yake, lakini sasa ni wauaji!
La ciudad recta se ha vuelto una prostituta; hubo un momento en que sus jueces tomaron decisiones correctas, cuando la justicia tenía un lugar de descanso en ella, pero ahora está llena de asesinos.
22 Fedha yenu imekuwa takataka, divai yenu nzuri imechanganywa na maji.
Tu plata ya no es metal verdadero, tu vino se mezcla con agua.
23 Watawala wenu ni waasi, rafiki wa wevi, wote wanapenda rushwa na kukimbilia hongo. Hawatetei yatima, shauri la mjane haliletwi mbele yao lisikilizwe.
Tus jefes se han ido contra el Señor, se han hecho amigos de los ladrones; Cada uno de ellos está buscando ganancias y persiguiendo recompensas; no toman las decisiones correctas para el niño que no tiene padre, y no les importa la causa de la viuda.
24 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mwenye Nguvu wa Israeli, asema hivi: “Lo, nitapata faraja kutoka kwa adui zangu na kujilipizia kisasi juu ya watesi wangu.
Por esta razón el Señor, el Señor de los ejércitos, el Fuerte de Israel, ha dicho: Pondré fin a mis enemigos y enviaré castigo a los que están contra mía;
25 Nitauelekeza mkono wangu dhidi yenu, nitawasafisha takataka zenu zote na kuwaondolea unajisi wenu wote.
Y mi mano volverá a estar sobre ti, lavando lo que es impuro con jabón, y quitando todo tu metal falso;
26 Nitawarudishia waamuzi wenu kama ilivyokuwa siku za zamani, nao washauri wenu kama ilivyokuwa mwanzoni. Baadaye utaitwa, Mji wa Haki, Mji Mwaminifu.”
Y les daré de nuevo jueces como al principio, y sabios guías como en el pasado; entonces serás nombrado, El Pueblo de Justicia, el verdadero pueblo.
27 Sayuni itakombolewa kwa haki, wale waliomo ndani yake waliotubu kwa uaminifu.
Los actos de arrepentimiento serán el precio del perdón de Sión, y por la justicia los hombres vivirán allí.
28 Lakini waasi na wenye dhambi wote wataangamizwa, nao wanaomwacha Bwana wataangamia.
Pero una destrucción común superará a los pecadores y los malhechores juntos, y los que se han alejado del Señor serán cortados.
29 “Mtaaibika kwa sababu ya hiyo mialoni ambayo mlifurahia, mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizozichagua.
Porque ellos serás avergonzado por los árboles que amaste y por los jardines que han escogido.
30 Mtakuwa kama mwaloni wenye majani yanayonyauka, kama bustani isiyokuwa na maji.
Porque serán como un árbol cuyas hojas se han secado, y como un jardín sin agua.
31 Mtu mwenye nguvu atatoweka kama majani makavu yawakayo moto, na kazi yake kama cheche ya moto; vyote vitaungua pamoja, wala hakuna wa kuuzima huo moto.”
Y los fuertes serán como estopa para el fuego, y su obra como una llama; y serán quemados juntos, sin nadie que apague el fuego.