< Isaya 1 >

1 Maono kuhusu Yuda na Yerusalemu ambayo Isaya mwana wa Amozi aliyaona wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.
The visioun, ether profesie, of Ysaie, the sone of Amos, which he siy on Juda and Jerusalem, in the daies of Osie, of Joathan, of Achas, and of Ezechie, kyngis of Juda.
2 Sikieni, enyi mbingu! Sikilizeni, enyi dunia! Kwa maana Bwana amesema: “Nimewalisha watoto na kuwalea, lakini wameniasi mimi.
Ye heuenes, here, and thou erthe, perseyue with eeris, for the Lord spak. Y haue nurschid and Y haue enhaunsid sones; sotheli thei han dispisid me.
3 Ngʼombe anamjua bwana wake, naye punda anajua hori la mmiliki wake, lakini Israeli hajui, watu wangu hawaelewi.”
An oxe knew his lord, and an asse knew the cratche of his lord; but Israel knewe not me, and my puple vndurstood not.
4 Lo! Taifa lenye dhambi, watu waliolemewa na uovu, uzao wa watenda mabaya, watoto waliozoelea upotovu! Wamemwacha Bwana, Wamemkataa kwa dharau yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli na kumgeuzia kisogo.
Wo to the synful folk, to the puple heuy in wickidnesse, to the weiward seed, to the cursid sones; thei han forsake the Lord, thei han blasfemyd the hooli of Israel, thei ben aliened bacward.
5 Kwa nini mzidi kupigwa? Kwa nini kudumu katika uasi? Kichwa chako chote kimejeruhiwa, moyo wako wote ni mgonjwa.
On what thing schal Y smyte you more, that encreessen trespassyng? Ech heed is sijk, and ech herte is morenynge.
6 Kutoka wayo wako wa mguu hadi kwenye utosi wa kichwa chako hakuna uzima: ni majeraha matupu na makovu na vidonda vitokavyo damu, havikusafishwa au kufungwa wala kulainishwa kwa mafuta.
Fro the sole of the foot til to the nol, helthe is not ther ynne; wounde, and wannesse, and betyng bolnynge is not boundun aboute, nether curid bi medicyn, nether nurschid with oile.
7 Nchi yenu imekuwa ukiwa, miji yenu imeteketezwa kwa moto; nchi yenu imeachwa tupu na wageni mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile imepinduliwa na wageni.
Youre lond is forsakun, youre citees ben brent bi fier; aliens deuouren youre cuntrei bifore you, and it schal be disolat as in the distriyng of enemyes.
8 Binti Sayuni ameachwa kama kipenu katika shamba la mizabibu, kama kibanda katika shamba la matikitimaji, kama mji uliohusuriwa.
And the douytir of Sion, `that is, Jerusalem, schal be forsakun as a schadewynge place in a vyner, and as an hulke in a place where gourdis wexen, and as a citee which is wastid.
9 Kama Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asingelituachia walionusurika, tungelikuwa kama Sodoma, tungelifanana na Gomora.
If the Lord of oostis hadde not left seed to vs, we hadden be as Sodom, and we hadden be lijk as Gomorre.
10 Sikieni neno la Bwana, ninyi watawala wa Sodoma; sikilizeni sheria ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora!
Ye princes of men of Sodom, here the word of the Lord; and ye puple of Gommorre, perseyue with eeris the lawe of youre God.
11 Bwana anasema, “Wingi wa sadaka zenu, ni kitu gani kwangu? Ninazo sadaka za kuteketezwa nyingi kupita kiasi, za kondoo dume na mafuta ya wanyama walionona. Sipendezwi na damu za mafahali wala za wana-kondoo na mbuzi.
Wherto offren ye to me the multitude of youre sacrifices? seith the Lord. Y am ful; Y wolde not the brent sacrifices of wetheris, and the ynnere fatnesse of fatte beestis, and the blood of calues, and of lambren, and of buckis of geet.
12 Mnapokuja kujihudhurisha mbele zangu, ni nani aliyewataka ninyi mfanye hivyo, huku kuzikanyaga nyua zangu?
Whanne ye camen bifore my siyt, who axide of youre hondis these thingis, that ye schulden go in myn hallys?
13 Acheni kuniletea sadaka zisizokuwa na maana! Uvumba wenu ni chukizo kwangu. Miandamo ya Mwezi, Sabato na makusanyiko ya ibada: siwezi kuvumilia makusanyiko yenu maovu.
Offre ye no more sacrifice in veyn; encense is abhomynacioun to me; Y schal not suffre neomenye, and sabat, and othere feestis.
14 Sikukuu zenu za Miandamo ya Mwezi, na sikukuu zenu zilizoamriwa: moyo wangu unazichukia. Zimekuwa mzigo kwangu, nimechoka kuzivumilia.
Youre cumpenyes ben wickid; my soule hatith youre calendis and youre solempnytees; tho ben maad diseseful to me, Y trauelide suffrynge.
15 Mnaponyoosha mikono yenu katika maombi, nitaficha macho yangu nisiwaone; hata mkiomba maombi mengi sitasikiliza. Mikono yenu imejaa damu;
And whanne ye stretchen forth youre hondis, Y schal turne awei myn iyen fro you; and whanne ye multiplien preyer, Y schal not here; for whi youre hondis ben ful of blood.
16 jiosheni na mkajitakase. Yaondoeni matendo yenu maovu mbele zangu! Acheni kutenda mabaya,
Be ye waischun, be ye clene; do ye awei the yuel of youre thouytis fro myn iyen; ceesse ye to do weiwardli, lerne ye to do wel.
17 jifunzeni kutenda mema! Tafuteni haki, watieni moyo walioonewa. Teteeni shauri la yatima, wateteeni wajane.
Seke ye doom, helpe ye hym that is oppressid, deme ye to the fadirles and modirles child, defende ye a widewe.
18 “Njooni basi tuhojiane,” asema Bwana. “Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu, zitakuwa nyeupe kama theluji; ingawa ni nyekundu sana kama damu, zitakuwa nyeupe kama sufu.
And come ye, and repreue ye me, seith the Lord. Thouy youre synnes ben as blood reed, tho schulen be maad whijt as snow; and thouy tho ben reed as vermylioun, tho schulen be whijt as wolle.
19 Kama mkikubali na kutii, mtakula mema ya nchi,
If ye wolen, and heren me, ye schulen ete the goodis of erthe.
20 lakini kama mkikataa na kuasi, mtaangamizwa kwa upanga.” Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena.
That if ye nylen, and ye terren me to wrathfulnesse, swerd schal deuoure you; for whi the mouth of the Lord spak.
21 Tazama jinsi mji uliokuwa mwaminifu umekuwa kahaba! Mwanzoni ulikuwa umejaa unyofu, haki ilikuwa inakaa ndani yake, lakini sasa ni wauaji!
Hou is the feithful citee ful of dom maad an hoore? riytfulnesse dwellide ther ynne; but now menquelleris dwellen ther ynne.
22 Fedha yenu imekuwa takataka, divai yenu nzuri imechanganywa na maji.
Thi siluer is turned in to dros, ether filthe; thi wyn is medlid with watir.
23 Watawala wenu ni waasi, rafiki wa wevi, wote wanapenda rushwa na kukimbilia hongo. Hawatetei yatima, shauri la mjane haliletwi mbele yao lisikilizwe.
Thi princes ben vnfeithful, the felowis of theuys; alle louen yiftis, suen meedis; thei demen not to a fadirles child, and the cause of a widewe entrith not to hem.
24 Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mwenye Nguvu wa Israeli, asema hivi: “Lo, nitapata faraja kutoka kwa adui zangu na kujilipizia kisasi juu ya watesi wangu.
For this thing, seith the Lord God of oostis, the stronge of Israel, Alas! Y schal be coumfortid on myn enemyes, and Y schal be vengid on myn enemyes.
25 Nitauelekeza mkono wangu dhidi yenu, nitawasafisha takataka zenu zote na kuwaondolea unajisi wenu wote.
And Y schal turne myn hond to thee, and Y schal sethe out thi filthe to the cleene, and Y schal do awei al thi tyn.
26 Nitawarudishia waamuzi wenu kama ilivyokuwa siku za zamani, nao washauri wenu kama ilivyokuwa mwanzoni. Baadaye utaitwa, Mji wa Haki, Mji Mwaminifu.”
And Y schal restore thi iuges, as thei weren bifor to, and thi counselours, as in elde tyme. Aftir these thingis thou schalt be clepid the citee of the riytful, a feithful citee.
27 Sayuni itakombolewa kwa haki, wale waliomo ndani yake waliotubu kwa uaminifu.
Sion schal be ayen bouyt in dom, and thei schulen bringe it ayen in to riytfulnesse;
28 Lakini waasi na wenye dhambi wote wataangamizwa, nao wanaomwacha Bwana wataangamia.
and God schal al to-breke cursid men and synneris togidere, and thei that forsoken the Lord, schulen be wastid.
29 “Mtaaibika kwa sababu ya hiyo mialoni ambayo mlifurahia, mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizozichagua.
For thei schulen be aschamed of idols, to whiche thei maden sacrifice; and ye shulen be aschamid on the orcherdis, whiche ye chesiden.
30 Mtakuwa kama mwaloni wenye majani yanayonyauka, kama bustani isiyokuwa na maji.
Whanne ye schulen be as an ook, whanne the leeues fallen doun, and as an orcherd with out watir.
31 Mtu mwenye nguvu atatoweka kama majani makavu yawakayo moto, na kazi yake kama cheche ya moto; vyote vitaungua pamoja, wala hakuna wa kuuzima huo moto.”
And youre strengthe schal be as a deed sparcle of bonys, `ether of herdis of flex, and youre werk schal be as a quyk sparcle; and euer either schal be brent togidere, and noon schal be that schal quenche.

< Isaya 1 >