< Hosea 9 >

1 Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
Ne veseli se, oh Izrael, zaradi radosti kakor drugo ljudstvo, kajti šel si vlačugarsko od svojega Boga, ljubil si nagrado na vsakem žitnem mlatišču.
2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
Mlatišče in vinska stiskalnica jih ne bosta hranila in novo vino se bo pokvarilo v njej.
3 Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
Ne bodo prebivali v Gospodovi deželi, temveč se bo Efrájim vrnil v Egipt in v Asiriji bodo jedli nečiste stvari.
4 Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
Ne bodo več darovali vinskih daritev Gospodu niti mu ne bodo ugajale. Njihove klavne daritve jim bodo kakor kruh žalovalcev. Vsi, ki bodo jedli od njih, bodo oskrunjeni, kajti njihov kruh, za njihovo dušo, ne bo prišel v Gospodovo hišo.
5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
Kaj boste storili na slovesen dan in na dan Gospodovega praznika?
6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
Kajti glej, odšli so zaradi uničenja. Egipt jih bo zbral, Memfis jih bo pokopal. Prijetne kraje za njihovo srebro bodo imele koprive v lasti, trnje bo v njihovih šotorskih svetiščih.
7 Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
Prišli so dnevi obiskanja, prišli so dnevi povračila, Izrael bo to vedel. Prerok je bedak, duhoven človek je zmešan zaradi množice tvoje krivičnosti in velikega sovraštva.
8 Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
Efrájimov stražar je bil z mojim Bogom, toda prerok je ptičarjeva zanka na vseh njegovih poteh in sovraštvo v hiši njegovega Boga.
9 Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
Globoko so se izpridili, kakor v dneh Gíbee, zato se bo spomnil njihove krivičnosti, obiskal bo njihove grehe.
10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
»Izraela sem našel podobnega trtam v divjini. Vaše očete sem videl kakor prvi sad na figovem drevesu ob njegovem prvem času, toda odšli so k Báal Peórju in se oddvojili v to sramoto in njihove ogabnosti so bile glede na to, kar so ljubili.
11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
Glede Efrájima, njihova slava bo odletela proč kakor ptica, od poroda in od maternice in od spočetja.
12 Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
Čeprav bodo vzredili svoje otroke, jih bom vendar oropal, da tam noben človek ne bo ostal. Da, gorje tudi tistim, ko odidem od njih!
13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
Efrájim je, kakor sem videl Tir, zasajen na prijetnem kraju, toda Efrájim bo svoje otroke privedel k morilcu.«
14 Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
Daj jim, oh Gospod. Kaj hočeš dati? Daj jim maternico, ki splavlja in suhe prsi.
15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
»Vsa njihova zlobnost je v Gilgálu, kajti tam sem jih zasovražil. Zaradi zlobnosti njihovih početij jih bom pognal iz svoje hiše. Ne bom jih več ljubil. Vsi njihovi princi so puntarji.
16 Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
Efrájim je udarjen, njihova korenina je posušena, nobenega sadu ne bodo obrodili. Da, čeprav bodo obrodili, bom vendar ubil celó ljubljeni sad njihove maternice.«
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.
Moj Bog jih bo zavrgel, ker mu niso prisluhnili in oni bodo postopači med narodi.

< Hosea 9 >