< Hosea 9 >
1 Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
Israël, ne te réjouis point, et ne sois pas transporté de joie comme les peuples, de ce que tu t'es prostitué en abandonnant ton Dieu! Tu as aimé le salaire de la prostitution sur toutes les aires de froment.
2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
L'aire et la cuve ne les repaîtront point, et le vin doux leur manquera.
3 Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
Ils ne demeureront pas dans la terre de l'Éternel; Éphraïm retournera en Égypte, et ils mangeront en Assyrie un aliment souillé.
4 Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
Ils ne feront point à l'Éternel des libations de vin, et leurs sacrifices ne lui plairont pas. Ce leur sera comme le pain de deuil; tous ceux qui en mangent seront souillés. Car leur pain ne sera que pour eux-mêmes; il n'entrera point dans la maison de l'Éternel.
5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
Que ferez-vous aux jours solennels, aux jours des fêtes de l'Éternel?
6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
Car voici, ils s'en vont à cause de la désolation. L'Égypte les recueillera; Memphis les ensevelira. L'ortie possédera leurs joyaux d'argent; l'épine croîtra dans leurs tentes.
7 Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
Ils viennent, les jours du châtiment! Ils viennent, les jours de la rétribution! Israël le saura! Le prophète est fou; l'homme inspiré est insensé, à cause de la grandeur de ton iniquité et de ta grande rébellion!
8 Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
La sentinelle d'Éphraïm est avec mon Dieu; mais le prophète est un filet d'oiseleur sur toutes ses voies, un ennemi dans la maison de son Dieu.
9 Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
Ils se sont entièrement corrompus, comme aux jours de Guibea. L'Éternel se souviendra de leur iniquité; il punira leurs péchés!
10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
J'ai trouvé Israël comme des grappes dans le désert; j'ai vu vos pères comme le premier fruit d'un figuier qui commence. Mais ils sont allés vers Baal-Péor; ils se sont consacrés à une chose infâme, ils sont devenus abominables comme ce qu'ils ont aimé.
11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
La gloire d'Éphraïm s'envolera comme un oiseau: plus de naissance, plus de grossesse, plus de conception!
12 Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
S'ils élèvent leurs enfants, je les en priverai avant l'âge d'homme. Car malheur à eux aussi, quand je me retirerai d'eux!
13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
Éphraïm, partout où je regarde vers Tyr, est planté dans un beau séjour; mais Éphraïm mènera ses fils à celui qui les tuera.
14 Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
O Éternel! donne-leur ... Que leur donnerais-tu? ... Donne-leur le sein qui avorte, et les mamelles taries!
15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
Tout leur mal est à Guilgal; c'est là que je les hais. A cause de la malice de leurs œuvres, je les chasserai de ma maison; je ne continuerai plus à les aimer; tous leurs chefs sont des rebelles.
16 Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
Éphraïm est frappé, sa racine est devenue sèche; ils ne porteront plus de fruit; et s'ils ont des enfants, je ferai mourir le fruit précieux de leur sein.
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.
Mon Dieu les rejettera, parce qu'ils ne l'ont point écouté, et ils seront errants parmi les nations.