< Hosea 9 >

1 Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
Ne te réjouis pas, Israël, jusqu’à l’exultation, comme les peuples; car tu t’es prostitué, abandonnant ton Dieu. Tu as aimé les présents dans toutes les aires à froment.
2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
L’aire et la cuve ne les nourriront pas, et le moût les trompera.
3 Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
Ils ne demeureront pas dans le pays de l’Éternel; mais Éphraïm retournera en Égypte, et mangera en Assyrie ce qui est impur.
4 Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
Ils ne feront pas de libations de vin à l’Éternel, et leurs sacrifices ne lui seront pas agréables: ce sera pour eux comme le pain de deuil; tous ceux qui en mangeront se souilleront; car leur pain est pour eux-mêmes; il n’entrera pas dans la maison de l’Éternel.
5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
Que ferez-vous au jour de l’assemblée, et au jour de fête de l’Éternel?
6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
Car voici, ils s’en sont allés à cause de la dévastation: l’Égypte les rassemblera, Moph les enterrera. Ce qu’ils ont de précieux [en objets] d’argent, l’ortie les héritera; le chardon est dans leurs tentes.
7 Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
Ils arrivent, les jours de la visitation; ils arrivent, les jours de la récompense! Israël le saura. Le prophète est insensé, l’homme inspiré est fou, à cause de la grandeur de ton iniquité et de la grandeur de ton hostilité.
8 Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
Éphraïm est aux aguets, [regardant à d’autres] à côté de mon Dieu. Le prophète est un piège d’oiseleur sur tous ses chemins, une hostilité dans la maison de son Dieu.
9 Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
Ils se sont enfoncés dans la corruption comme aux jours de Guibha. Il se souviendra de leur iniquité, il visitera leurs péchés.
10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
J’ai trouvé Israël comme des raisins dans le désert; j’ai vu vos pères au commencement comme le premier fruit du figuier. Ils sont allés à Baal-Péor, et ils se sont voués à cette honteuse [idole], et sont devenus abominables comme leur amant.
11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
Quant à Éphraïm, leur gloire s’envolera comme un oiseau; … point d’enfantement, point de grossesse, point de conception!
12 Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
Quand même ils élèveraient leurs fils, je les priverais de fils, en sorte qu’il n’y ait pas d’homme. Car aussi, malheur à eux, lorsque je me serai retiré d’eux!
13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
Éphraïm, comme je l’ai vu, a été une Tyr plantée dans une campagne agréable; mais Éphraïm doit mener dehors ses fils au meurtrier.
14 Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
Donne-leur, Éternel! Que donneras-tu? Donne-leur un sein qui avorte et des mamelles desséchées.
15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
Toute leur méchanceté est à Guilgal, car là, je les ai haïs; à cause de la méchanceté de leurs actions, je les chasserai de ma maison. Je ne les aimerai plus. Tous leurs princes sont des rebelles.
16 Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
Éphraïm a été frappé: leur racine a séché, ils ne produiront pas de fruit. Si même ils enfantent, je ferai mourir le fruit précieux de leur sein.
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.
Mon Dieu les a rejetés, car ils ne l’ont pas écouté, et ils seront errants parmi les nations.

< Hosea 9 >