< Hosea 9 >
1 Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
“Do not rejoice, O Israel, do not be joyful like the peoples, For you have gone whoring from your God, You have loved a wage near all floors of grain.
2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
Floor and winepress do not feed them, And new wine fails in her,
3 Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
They do not abide in the land of YHWH, And Ephraim has turned back [to] Egypt, And they eat an unclean thing in Asshur.
4 Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
They do not pour out wine to YHWH, Nor are they sweet to Him, Their sacrifices [are] as bread of mourners to them, All eating it are unclean: For their bread [is] for themselves, It does not come into the house of YHWH.
5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
What do you do at the day appointed? And at the day of YHWH’s festival?
6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
For behold, they have gone because of destruction, Egypt gathers them, Moph buries them, The desirable things of their silver, Nettles possess them—a thorn [is] in their tents.
7 Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
The days of inspection have come in, The days of repayment have come in, Israel knows! The prophet [is] a fool, Mad [is] the man of the spirit, Because of the abundance of your iniquity, And great [is] the hatred.
8 Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
Ephraim is looking [away] from My God, The prophet! A snare of a fowler [is] over all his ways, Hatred [is] in the house of his God.
9 Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
They have gone deep—have done corruptly, As [in] the days of Gibeah, He remembers their iniquity, He inspects their sins.
10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
As grapes in a wilderness I found Israel, As the first-fruit in a fig tree, at its beginning, I have seen your fathers, They have gone in [to] Ba‘al-Peor, And are separated to a shameful thing, And have become abominable like their love.
11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
Ephraim [is] as a bird, their glory flies away, without birth, and without womb, and without conception.
12 Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
For though they nourish their sons, I have made them childless—without man, Surely also, woe to them when I turn aside from them.
13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
Ephraim! When I have looked to the rock, Is planted in comeliness, And Ephraim [is] to bring out his sons to a slayer.
14 Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
Give to them, YHWH—what do You give? Give to them miscarrying womb, and dry breasts.
15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
All their evil [is] in Gilgal, Surely there I have hated them, Because of the evil of their doings, Out of My house I drive them, I no longer love them, All their heads [are] apostates.
16 Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
Ephraim has been struck, Their root has dried up, they do not yield fruit, Indeed, though they bring forth, I have put to death the desired of their womb.
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.
My God rejects them, Because they have not listened to Him, And they are wanderers among nations!”