< Hosea 9 >

1 Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
Rejoice not, O Israel, unto exultation, like the peoples, for thou hast gone astray from thy God, thou hast loved a harlot's hire upon every corn-floor.
2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
The threshing-floor and the wine-press shall not feed them, and the new wine shall fail her.
3 Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
They shall not dwell in the LORD'S land; but Ephraim shall return to Egypt, and they shall eat unclean food in Assyria.
4 Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
They shall not pour out wine-offerings to the LORD, neither shall they be pleasing unto Him; their sacrifices shall be unto them as the bread of mourners, all that eat thereof shall be polluted; for their bread shall be for their appetite, it shall not come into the house of the LORD.
5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
What will ye do in the day of the appointed season, and in the day of the feast of the LORD?
6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
For, lo, they are gone away from destruction, yet Egypt shall gather them up, Memphis shall bury them; their precious treasures of silver, nettles shall possess them, thorns shall be in their tents.
7 Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
The days of visitation are come, the days of recompense are come, Israel shall know it. The prophet is a fool, the man of the spirit is mad! For the multitude of thine iniquity, the enmity is great.
8 Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
Ephraim is a watchman with my God; as for the prophet, a fowler's snare is in all his ways, and enmity in the house of his God.
9 Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
They have deeply corrupted themselves, as in the days of Gibeah; He will remember their iniquity, He will punish their sins.
10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
I found Israel like grapes in the wilderness, I saw your fathers as the first-ripe in the fig-tree at her first season; but so soon as they came to Baal-peor, they separated themselves unto the shameful thing, and became detestable like that which they loved.
11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
As for Ephraim, their glory shall fly away like a bird; there shall be no birth, and none with child, and no conception.
12 Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
Yea, though they bring up their children, yet will I bereave them, that there be not a man left; yea, woe also to them when I depart from them!
13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
Ephraim, like as I have seen Tyre, is planted in a pleasant place; but Ephraim shall bring forth his children to the slayer.
14 Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
Give them, O LORD, whatsoever Thou wilt give; give them a miscarrying womb and dry breasts.
15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
All their wickedness is in Gilgal, for there I hated them; because of the wickedness of their doings I will drive them out of My house; I will love them no more, all their princes are rebellious.
16 Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
Ephraim is smitten, their root is dried up, they shall bear no fruit; yea, though they bring forth, yet will I slay the beloved fruit of their womb.
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.
My God will cast them away, because they did not hearken unto Him; and they shall be wanderers among the nations.

< Hosea 9 >