< Hosea 9 >
1 Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
Israel, don't rejoice! Don't celebrate like other nations! For you have practiced prostitution; you have loved a prostitute's wages on every threshing floor of grain.
2 Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
Your threshing floors and winepresses will not feed you; the land will fail to produce your new wine.
3 Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
You will not stay in the Lord's land, instead Ephraim will return to Egypt, and will eat unclean food in Assyria.
4 Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
You won't pour out any drink offerings to the Lord. None of your sacrifices will please him. Your sacrifices will be like food eaten by a person in mourning—all who eat will be unclean. You will eat this food yourselves, but it will not enter the house of the Lord.
5 Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
What are you going to do on the days of your appointed religious feasts, on the days of the festivals of the Lord?
6 Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
Look, they have left because of the destruction: Egypt with gather them, and Memphis will bury them. They gain a “valued possession” for their silver. Weeds will possess them, and thorns will grow over their tents.
7 Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
The time of punishment has come; the day of retribution has arrived. Let Israel know! You say the prophet is a fool, the man of the Spirit is mad, because your sin and hostility is so great.
8 Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
The watchman over Ephraim is with my God, and a prophet is a birdcatcher's snare on all his ways. Hatred is in the house of his God
9 Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
for they have corrupted themselves so deeply, as in the time of Gibeah. He will remember their sin; he will punish their wickedness.
10 “Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
When I found Israel, it was like finding grapes in the desert. When I saw your forefathers it was like seeing early fruit on the fig tree. But when they came to Baal Peor, they gave themselves over to that shameful idol, becoming as filthy as the filthy thing they loved.
11 Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
Ephraim! Like a bird that flies away so shall your glory—no births, no pregnancies, no conceptions.
12 Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
Even if they bring up children, I will make sure they do not survive. What a disaster for you when I turn away from you!
13 Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
Ephraim! Just as I saw Tyre planted in a meadow, so too Ephraim will lead out his children to the murderer.
14 Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
Give them—well, Lord, what should you give them? Give them wombs that miscarry and dry breasts.
15 “Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
All of their evil began at Gilgal, and that's where I began to hate them. I will drive them out of my house because of their wickedness. I will love them no longer; all their leaders are rebels.
16 Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
Ephraim, you are blighted, dried up from the roots. You shall bear no fruit. Even if you have children, I will slaughter your beloved offspring.
17 Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.
My God will reject you because you have not listened to him, and you will become homeless wanderers among the nations.