< Hosea 8 >

1 “Wekeni tarumbeta midomoni mwenu! Tai yuko juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja Agano langu, wameasi dhidi ya sheria yangu.
“¡Pon la trompeta en tus labios! Algo así como un águila está sobre la casa de Yahvé, porque han roto mi pacto y se rebelaron contra mi ley.
2 Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’
Me gritan: ‘¡Dios mío, nosotros, Israel, te reconocemos!
3 Lakini Israeli amekataa lile lililo jema, adui atamfuatia.
Israel ha abandonado lo que es bueno. El enemigo lo perseguirá.
4 Wanaweka wafalme bila idhini yangu, wamechagua wakuu bila kibali changu. Kwa fedha zao na dhahabu wamejitengenezea sanamu kwa ajili ya maangamizi yao wenyewe.
Han puesto reyes, pero no por mí. Han hecho príncipes, y yo no lo he aprobado. De su plata y su oro se han hecho ídolos, para que sean cortados.
5 Ee Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama! Hasira yangu inawaka dhidi yao. Watakuwa najisi mpaka lini?
¡Que Samaria arroje su ídolo del becerro! ¡Mi ira arde contra ellos! ¿Cuánto tiempo pasará hasta que sean capaces de la pureza?
6 Zimetoka katika Israeli! Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu. Atavunjwa vipande vipande, yule ndama wa Samaria.
¡Pues esto es incluso de Israel! El obrero lo hizo, y no es Dios; En efecto, el becerro de Samaria será despedazado.
7 “Wanapanda upepo na kuvuna upepo wa kisulisuli. Bua halina suke, halitatoa unga. Kama lingetoa nafaka, wageni wangeila yote.
Porque ellos siembran el viento, y cosecharán el torbellino. No tiene grano en pie. El tallo no producirá ninguna cabeza. Si cede, los extraños se lo tragarán.
8 Israeli amemezwa; sasa yupo miongoni mwa mataifa kama kitu kisicho na thamani.
Israel es tragado. Ahora están entre las naciones como una cosa sin valor.
9 Kwa kuwa wamepanda kwenda Ashuru kama punda-mwitu anayetangatanga peke yake. Efraimu amejiuza mwenyewe kwa wapenzi.
Porque han subido a Asiria, como un burro salvaje que vaga solo. Efraín ha contratado amantes para sí mismo.
10 Ingawa wamejiuza wenyewe miongoni mwa mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wataanza kudhoofika chini ya uonevu wa mfalme mwenye nguvu.
Pero aunque se vendieron entre las naciones, Ahora los reuniré; y comienzan a consumirse a causa de la opresión del rey de los poderosos.
11 “Ingawa Efraimu alijenga madhabahu nyingi kwa ajili ya sadaka za dhambi, hizi zimekuwa madhabahu za kufanyia dhambi.
Porque Efraín ha multiplicado los altares para pecar, se convirtieron para él en altares para pecar.
12 Nimeandika kwa ajili yao mambo mengi kuhusu sheria yangu, lakini wameziangalia kama kitu cha kigeni.
Le escribí las muchas cosas de mi ley, pero fueron considerados como algo extraño.
13 Wanatoa dhabihu nilizopewa mimi nao wanakula hiyo nyama, lakini Bwana hapendezwi nao. Sasa ataukumbuka uovu wao na kuadhibu dhambi zao: Watarudi Misri.
En cuanto a los sacrificios de mis ofrendas, sacrifican carne y la comen, pero Yahvé no los acepta. Ahora se acordará de su iniquidad, y castigar sus pecados. Volverán a Egipto.
14 Israeli amemsahau Muumba wake na kujenga majumba ya kifalme, Yuda amejengea miji mingi ngome. Lakini nitatuma moto kwenye miji yao utakaoteketeza ngome zao.”
Porque Israel se ha olvidado de su Hacedor y ha construido palacios; y Judá ha multiplicado las ciudades fortificadas; pero yo enviaré un fuego sobre sus ciudades, y devorará sus fortalezas”.

< Hosea 8 >