< Hosea 8 >
1 “Wekeni tarumbeta midomoni mwenu! Tai yuko juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja Agano langu, wameasi dhidi ya sheria yangu.
“Place a trumpet at your lips! An eagle is coming over the house of Yahweh because the people have broken my covenant and rebelled against my law.
2 Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’
They cry out to me, 'My God, we in Israel know you.'
3 Lakini Israeli amekataa lile lililo jema, adui atamfuatia.
But Israel has rejected what is good, and the enemy will pursue him.
4 Wanaweka wafalme bila idhini yangu, wamechagua wakuu bila kibali changu. Kwa fedha zao na dhahabu wamejitengenezea sanamu kwa ajili ya maangamizi yao wenyewe.
They have set up kings, but not by me. They have made princes, but without my knowledge. With their silver and gold they have made idols for themselves, but it was only so they might be cut off.”
5 Ee Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama! Hasira yangu inawaka dhidi yao. Watakuwa najisi mpaka lini?
“Your calf has been rejected, Samaria. My anger is burning against these people. For how long will they stay guilty?
6 Zimetoka katika Israeli! Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu. Atavunjwa vipande vipande, yule ndama wa Samaria.
For this idol came from Israel; a workman made it; it is not God! The calf of Samaria will be broken to pieces.
7 “Wanapanda upepo na kuvuna upepo wa kisulisuli. Bua halina suke, halitatoa unga. Kama lingetoa nafaka, wageni wangeila yote.
For the people sow the wind and reap the whirlwind. The standing grain has no heads; it yields no flour. If it does come to maturity, foreigners will devour it.
8 Israeli amemezwa; sasa yupo miongoni mwa mataifa kama kitu kisicho na thamani.
Israel is swallowed up; now they lie among the nations like something useless.
9 Kwa kuwa wamepanda kwenda Ashuru kama punda-mwitu anayetangatanga peke yake. Efraimu amejiuza mwenyewe kwa wapenzi.
For they went up to Assyria like a wild donkey all alone. Ephraim has hired lovers for herself.
10 Ingawa wamejiuza wenyewe miongoni mwa mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wataanza kudhoofika chini ya uonevu wa mfalme mwenye nguvu.
Even though they have hired lovers among the nations, I will now gather them together. They will begin to waste away because of the oppression of the king of princes.
11 “Ingawa Efraimu alijenga madhabahu nyingi kwa ajili ya sadaka za dhambi, hizi zimekuwa madhabahu za kufanyia dhambi.
For Ephraim has multiplied altars for sin offerings, but they have become altars for committing sins instead.
12 Nimeandika kwa ajili yao mambo mengi kuhusu sheria yangu, lakini wameziangalia kama kitu cha kigeni.
I could write down my law for them ten thousand times, but they would view it as something strange to them.
13 Wanatoa dhabihu nilizopewa mimi nao wanakula hiyo nyama, lakini Bwana hapendezwi nao. Sasa ataukumbuka uovu wao na kuadhibu dhambi zao: Watarudi Misri.
As for the sacrifices of my offerings, they sacrifice meat and eat it, but I, Yahweh, do not accept them. Now I will think about their iniquity and punish their sins. They will return to Egypt.
14 Israeli amemsahau Muumba wake na kujenga majumba ya kifalme, Yuda amejengea miji mingi ngome. Lakini nitatuma moto kwenye miji yao utakaoteketeza ngome zao.”
Israel has forgotten me, his Maker, and has built palaces. Judah has fortified many cities, but I will send fire on his cities; it will destroy his fortresses.