< Hosea 7 >

1 kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
Quand j'ai voulu guérir Israël, alors s'est révélée l'iniquité d'Ephraïm, et la méchanceté de Samarie; car ils pratiquent le mensonge; le voleur pénètre dans la maison, le brigand se répand au dehors.
2 lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
Et ils ne disent pas en leurs cœurs que je me souviens de toute leur méchanceté. Maintenant leurs forfaits les entourent, ils sont là devant moi.
3 “Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
Ils égaient le roi par leur méchanceté, et les princes par leurs mensonges.
4 Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
Ils sont tous adultères, pareils à un four allumé par le boulanger, qui cesse d'attiser le feu, depuis qu'il a pétri la pâte jusqu'à ce qu'elle soit levée.
5 Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
Au jour de notre roi, les princes se rendent malades par la chaleur du vin; il a étendu sa main avec les moqueurs.
6 Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
Car, dans leur complot, ils ont mis leurs cœurs comme dans un four. Leur boulanger a dormi toute la nuit; le matin, il a été embrasé comme une flamme ardente.
7 Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
Tous sont chauffés comme un four, et ils dévorent leurs juges. Tous leur rois sont tombés, sans qu'aucun d'eux ait crié vers moi.
8 “Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
Ephraïm se mêle avec les peuples; Ephraïm est un gâteau qu'on n'a pas retourné.
9 Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
Des étrangers ont dévoré sa force, et il ne le sait pas; des cheveux blancs parsèment sa tête, et il ne le sait pas.
10 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
L'orgueil d'Ephraïm témoigne contre lui; ils ne reviennent pas à Yahweh, leur Dieu, et ils ne le recherchent pas, malgré tout cela.
11 “Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
Ephraïm est devenu comme une colombe, simple et sans intelligence; ils invoquent l'Egypte, ils vont en Assyrie.
12 Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
Pendant qu'ils y vont, j'étends sur eux mon filet; je les ferai tomber comme les oiseaux du ciel, je les châtierai comme on l'a annoncé dans leur assemblée.
13 Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
Malheur à eux, car ils ont fui loin de moi! Ruine sur eux, car ils m'ont été infidèles! Et moi, je voudrais les sauver; mais eux disent contre moi des mensonges.
14 Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
Ils ne crient point vers moi dans leur cœur, quand ils se lamentent sur leurs couches. Ils se tourmentent au sujet du froment et du vin nouveau, se détournant de moi.
15 Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
Moi, je les instruisais et je fortifiais leurs bras, et ils méditent le mal contre moi.
16 Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.
Ils se tournent, mais non pas en haut; ils sont comme un arc trompeur; leurs chefs tomberont par l'épée à cause de la fureur de leurs langues; et cela fera rire d'eux au pays d'Egypte.

< Hosea 7 >