< Hosea 7 >

1 kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
Quand je guérirais Israël, alors l'iniquité d'Ephraïm est découverte, aussi la méchanceté de Samarie; car ils commettent des mensonges, et le voleur entre, et la bande de voleurs fait des ravages à l'extérieur.
2 lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
Ils ne considèrent pas dans leur cœur que je me souviens de toute leur méchanceté. Maintenant, leurs propres actes les ont engloutis. Ils sont devant mon visage.
3 “Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
Ils réjouissent le roi par leur méchanceté, et les princes avec leurs mensonges.
4 Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
Ils sont tous adultères. Ils brûlent comme un four que le boulanger cesse de remuer, du pétrissage de la pâte, jusqu'à ce qu'elle soit levée.
5 Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
Le jour de notre roi, les princes se sont rendus malades par la chaleur du vin. Il a joint sa main à celle des moqueurs.
6 Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
Car ils ont préparé leur cœur comme un four, pendant qu'ils sont à l'affût. Leur colère couve toute la nuit. Au matin, il brûle comme un feu ardent.
7 Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
Ils sont tous aussi chauds qu'un four, et dévoreront leurs juges. Tous leurs rois sont tombés. Il n'y a personne parmi eux qui m'appelle.
8 “Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
Ephraïm se mêle aux nations. Ephraïm est une crêpe non retournée.
9 Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
Des étrangers ont dévoré sa force, et il ne le réalise pas. En effet, les cheveux gris sont ici et là sur lui, et il ne le réalise pas.
10 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
L'orgueil d'Israël témoigne de sa face; mais ils ne sont pas retournés à Yahvé, leur Dieu, ni ne l'a cherché, pour tout cela.
11 “Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
« Ephraïm est comme une colombe facile à tromper, sans intelligence. Ils appellent l'Égypte. Ils vont en Assyrie.
12 Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
Quand ils partiront, j'étendrai mon filet sur eux. Je les ferai tomber comme les oiseaux du ciel. Je les châtierai, comme l'a entendu leur assemblée.
13 Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
Malheur à eux! Car ils se sont éloignés de moi. Destruction pour eux! Car ils m'ont offensé. Bien que je les rachète, mais ils ont dit des mensonges contre moi.
14 Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
Ils n'ont pas crié vers moi avec leur cœur, mais ils hurlent sur leur lit. Ils s'assemblent pour le grain et le vin nouveau. Ils se détournent de moi.
15 Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
Bien que j'aie enseigné et fortifié leurs bras, mais ils complotent le mal contre moi.
16 Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.
Ils reviennent, mais pas vers le Très-Haut. Ils sont comme un arc défectueux. Leurs princes tomberont par l'épée à cause de la rage de leur langue. Ce sera leur dérision dans le pays d'Égypte.

< Hosea 7 >