< Hosea 7 >
1 kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
When heal I Israel and it is revealed [the] iniquity of Ephraim and [the] evil deeds of Samaria for they do falsehood and a thief he comes it attacks a marauding band in the street.
2 lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
And not they say to heart their all evil their I remember now they have surrounded them deeds their before face my they are.
3 “Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
By evil their they make glad [the] king and by lies their princes.
4 Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
All of them [are] adulterers like an oven burning from a baker [who] he ceases stirring up from kneading [the] dough until is leavened it.
5 Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
[the] day of King our they became sick princes fever from wine he stretched out hand his with scorners.
6 Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
For they have brought near like oven heart their in ambush their all the night [is] sleeping baker their morning it [is] burning like a fire of flame.
7 Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
All of them they are hot like oven and they devour rulers their all kings their they have fallen there not [is one who] calls among them to me.
8 “Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
Ephraim among the peoples he he mixes himself Ephraim he has become a bread cake not turned over.
9 Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
They have consumed strangers strength his and he not he knows also gray hair it has sneaked in on him and he not he knows.
10 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
And it testifies [the] pride of Israel in face its and not they have returned to Yahweh God their and not they have sought him for all this.
11 “Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
And he has become Ephraim like a dove silly there not [is] heart Egypt they have called Assyria they have gone.
12 Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
Just when they will go I will spread over them net my like [the] bird[s] of the heavens I will bring down them I will chasten them according to a report to assembly their.
13 Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
Woe! to them for they have fled from me devastation [belongs] to them for they have transgressed against me and I I will redeem them and they they have spoken on me lies.
14 Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
And not they have cried out to me with heart their if they wail on beds their on grain and new wine they assemble themselves they turn aside against me.
15 Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
And I I instructed [them] I strengthened arms their and against me they plot evil.
16 Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.
They turn - not height they have become like a bow of slackness they will fall by the sword leaders their from [the] indignation of tongue their this [will be] mockery their in [the] land of Egypt.