< Hosea 7 >
1 kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
When I woulde haue healed Israel, then the iniquitie of Ephraim was discouered, and the wickednesse of Samaria: for they haue dealt falsly: and the theefe commeth in, and the robber spoyleth without.
2 lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
And they consider not in their hearts, that I remember all their wickednes: now their owne inuentions haue beset them about: they are in my sight.
3 “Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
They make the King glad with their wickednesse, and the princes with their lies.
4 Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
They are all adulterers, and as a very ouen heated by ye baker, which ceaseth from raysing vp, and from kneading ye dough vntill it be leauened.
5 Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
This is the day of our King: the princes haue made him sicke with flagons of wine: he stretcheth out his hand to scorners.
6 Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
For they haue made ready their heart like an ouen whiles they lie in waite: their baker sleepeth all the night: in the morning it burneth as a flame of fire.
7 Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
They are all hote as an ouen, and haue deuoured their iudges: all their Kings are fallen: there is none among them that calleth vnto me.
8 “Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
Ephraim hath mixt himselfe among the people. Ephraim is as a cake on the hearth not turned.
9 Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
Strangers haue deuoured his strength, and he knoweth it not: yea, gray heares are here and there vpon him, yet he knoweth not.
10 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
And the pride of Israel testifieth to his face, and they doe not returne to the Lord their God, nor seeke him for all this.
11 “Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
Ephraim also is like a doue deceiued, without heart: they call to Egypt: they go to Asshur.
12 Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
But when they shall go, I will spred my net vpon them, and drawe them downe as the foules of the heauen: I will chastice them as their congregation hath heard.
13 Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
Wo vnto them: for they haue fled away from me: destruction shalbe vnto them, because they haue transgressed against me: though I haue redeemed them, yet they haue spoken lyes against me.
14 Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
And they haue not cryed vnto me with their hearts, when they houled vpon their beds: they assembled themselues for corne, and wine, and they rebell against me.
15 Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
Though I haue boud and strengthened their arme, yet doe they imagine mischiefe against me.
16 Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.
They returne, but not to the most high: they are like a deceitfull bowe: their princes shall fall by the sword, for the rage of their tongues: this shall be their derision in the land of Egypt.