< Hosea 6 >
1 “Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
Allons, retournons à l’Eternel, car a-t-il déchiré, il nous guérira aussi, a-t-il frappé, il pansera nos blessures!
2 Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
Déjà au bout de deux jours il nous aura rendu la vie; le troisième jour il nous aura relevés, pour que nous subsistions devant lui.
3 Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
Tâchons de connaître, hâtons-nous de connaître l’Eternel: son apparition est certaine comme celle de l’aurore, il vient à nous comme la pluie, comme la pluie d’arrière-saison qui abreuve la terre.
4 “Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
Que dois-je faire pour toi, Ephraïm, que dois-je faire pour toi, Juda? votre amour est pourtant comme une nuée matinale, comme la rosée qui se dissipe de bonne heure.
5 Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
C’Est pourquoi je fais des trouées parmi les prophètes, je les fais périr par les paroles de ma bouche, et ainsi tes arrêts éclatent à la lumière.
6 Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.
C’Est que je prends plaisir à la bonté et non au sacrifice, je préfère la connaissance de Dieu aux holocaustes,
7 Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
tandis qu’eux à la façon des hommes ont transgressé l’alliance et, depuis lors, me sont devenus infidèles.
8 Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
Ghilead est une cité de malfaiteurs, pleine d’embûches meurtrières.
9 Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
Telles des bandes qui guettent le passant, telle est la troupe des prêtres: ils assassinent sur le chemin qui conduit à Sichem, tant ils commettent d’infamies!
10 Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
Dans la maison d’Israël, j’ai vu des choses horribles; là s’étale l’inconduite d’Ephraïm, là se déshonore Israël.
11 “Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,
A toi également, ô Juda, on te prépare une moisson, alors que je voulais réparer les pertes de mon peuple.