< Hosea 6 >
1 “Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
“Come, let us return to Yahweh. For he has torn us to pieces, but he will heal us; he has injured us, but he will bandage our wounds.
2 Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
After two days he will revive us; he will raise us up on the third day, and we will live before him.
3 Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
Let us know Yahweh; let us press on to know Yahweh. His coming out is as sure as the dawn; he will come to us like the showers, like the spring rains that water the land.”
4 “Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
Ephraim, what will I do with you? Judah, what will I do with you? Your faithfulness is like a morning cloud, like the dew that goes away early.
5 Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
So I have cut them to pieces by the prophets, I have killed them with the words of my mouth. Your decrees are like the light that shines out.
6 Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.
For I desire faithfulness and not sacrifice, and the knowledge of God more than burnt offerings.
7 Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
Like Adam they have broken the covenant; they were unfaithful to me.
8 Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
Gilead is a city of evildoers with footprints of blood.
9 Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
As gangs of robbers wait for someone, so the priests band together to commit murder on the way to Shechem; they have committed shameful crimes.
10 Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
In the house of Israel I have seen a horrible thing; Ephraim's prostitution is there, and Israel has become unclean.
11 “Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,
For you also, Judah, a harvest has been appointed, when I will restore the fortunes of my people.