< Hosea 6 >

1 “Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
“Come, and we turn back to YHWH, For He has torn, and He heals us, He strikes, and He binds us up.
2 Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
He revives us after two days, In the third day He raises us up, And we live before Him.
3 Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
And we know—we pursue to know YHWH, His going forth is prepared as the dawn, And He comes in as a shower to us, As spring rain [and] autumn rain to the earth.”
4 “Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
“What do I do to you, O Ephraim? What do I do to you, O Judah? Your goodness [is] as a cloud of the morning, And as dew rising early—going.
5 Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
Therefore I have hewed by prophets, I have slain them by sayings of My mouth, And My judgments go forth to the light.
6 Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.
For kindness I desired, and not sacrifice, And a knowledge of God above burnt-offerings.
7 Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
And they, as Adam, transgressed a covenant, There they dealt treacherously against Me.
8 Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
Gilead [is] a city of workers of iniquity, Slippery from blood.
9 Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
And as bands wait for a man, A company of priests murder—the way to Shechem, For they have done wickedness.
10 Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
In the house of Israel I have seen a horrible thing, There [is] the whoredom of Ephraim—Israel is defiled.
11 “Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,
Also, O Judah, a harvest is appointed to you, In My turning back [to] the captivity of My people!”

< Hosea 6 >