< Hosea 6 >

1 “Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
“Hajde, vratimo se Jahvi! On je razderao, on će nas iscijeliti: on je udario, on će nam poviti rane;
2 Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
poslije dva dana oživit će nas, trećeg će nas dana podignuti i mi ćemo živjeti pred njim.
3 Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
Težimo da upoznamo Jahvu: k'o zora pouzdan mu dolazak. On će nam doći poput dažda jesenskog, poput kiše proljetne što natapa zemlju.”
4 “Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
Što za tebe mogu učiniti, Efrajime? Što za tebe mogu učiniti, Judo? K'o oblak jutarnji ljubav je vaša, k'o rana rosa koje nestaje.
5 Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
Zato sam ih preko proroka sjekao i ubijao riječima usta svojih; al' sud će tvoj izaći k'o svjetlost.
6 Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.
Jer ljubav mi je mila, ne žrtve, poznavanje Boga, ne paljenice.
7 Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
Al' oni su kod Adama prekršili Savez i ondje mene iznevjerili.
8 Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
Gilead je grad zlikovački, pun krvavih tragova.
9 Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
Družba je svećenička kao zasjeda razbojnička: ubijaju na šekemskom putu; odista, sramotu počinjaju!
10 Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
Strahotu vidjeh u domu Izraelovu; Efrajim se ondje bludu odaje i skvrni se Izrael.
11 “Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,
I tebi sam, Judo, žetvu odredio kad okrenem udes naroda svoga.

< Hosea 6 >