< Hosea 5 >
1 “Sikieni hili, enyi makuhani! Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli! Sikieni, ee nyumba ya mfalme! Hukumu hii ni dhidi yenu: Mmekuwa mtego huko Mispa, wavu uliotandwa juu ya Tabori.
Entendez-le, sacrificateurs, écoute-le, maison d'Israël! et maison du roi, sois-y attentive! car pour vous il s'agit du jugement; car vous fûtes un filet à Mitspa, et une toile tendue sur le Thabor.
2 Waasi wamezidisha sana mauaji. Mimi nitawatiisha wote.
Ils accumulent les sacrifices coupables; mais moi [j'accumulerai] les châtiments sur eux tous.
3 Ninajua yote kuhusu Efraimu, Israeli hukufichika kwangu. Efraimu, sasa umegeukia ukahaba, Israeli amenajisika.
Je connais Éphraïm, et Israël ne m'est point caché; car maintenant tu te prostitues, Éphraïm, et Israël se souille.
4 “Matendo yao hayawaachii kurudi kwa Mungu wao. Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao, hawamkubali Bwana.
Ils ne font point leur œuvre de revenir à leur Dieu, car l'esprit d'impudicité est en eux, et de l'Éternel ils n'ont nulle connaissance.
5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao; Waisraeli, hata Efraimu, wanajikwaa katika dhambi zao; pia Yuda atajikwaa pamoja nao.
Ainsi l'orgueil d'Israël s'exprime sur son visage, et Israël et Éphraïm tomberont par l'effet de leur péché; avec eux tombera aussi Juda.
6 Wakati wanapokwenda na makundi yao ya kondoo na ngʼombe kumtafuta Bwana, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.
Avec leurs brebis et leurs taureaux ils viendront chercher l'Éternel et ne le trouveront pas; Il se dérobe à eux.
7 Wao si waaminifu kwa Bwana; wamezaa watoto haramu. Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi zitawaangamiza wao pamoja na mashamba yao.
A l'Éternel ils furent infidèles; car ils donnèrent naissance à des enfants bâtards; maintenant il ne faudra qu'une nouvelle lune pour les dévorer, eux et leurs possessions.
8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea, baragumu huko Rama. Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni, ongoza, ee Benyamini.
Sonnez de la trompette en Guibha, et du clairon à Rama! pousse des cris, Bethaven! on est à ta poursuite, Benjamin!
9 Efraimu ataachwa ukiwa katika siku ya kuadhibiwa. Miongoni mwa makabila ya Israeli ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.
Éphraïm sera un désert au jour du châtiment; parmi les tribus d'Israël j'annonce une chose certaine.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mawe ya mpaka. Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama mafuriko ya maji.
Les princes de Juda sont comme ceux qui déplacent les bornes; sur eux je verserai comme les eaux ma colère.
11 Efraimu ameonewa, amekanyagwa katika hukumu kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.
Éphraïm est accablé, écrasé par le jugement, car il se plaît à suivre la voie qu'il se trace.
12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa watu wa Yuda.
Et je suis comme une teigne pour Éphraïm, comme une carie pour la maison de Juda.
13 “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake, naye Yuda vidonda vyake, ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru, na kuomba msaada kwa mfalme mkuu. Lakini hawezi kukuponya, wala hawezi kukuponya vidonda vyako.
Et Éphraïm voit sa maladie, et Juda sa blessure, et Éphraïm se rend auprès d'Assur, et députe vers un roi qui le venge; mais il ne pourra vous guérir, ni enlever votre plaie.
14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu, kama simba mkubwa kwa Yuda. Nitawararua vipande vipande na kuondoka; nitawachukua mbali, na hakuna wa kuwaokoa.
Car je suis comme un lion pour Éphraïm, et comme un jeune lion pour la maison de Juda; moi, moi je déchire, puis je m'en vais, j'emporte, et personne qui sauve.
15 Kisha nitarudi mahali pangu mpaka watakapokubali kosa lao. Nao watautafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”
Je m'en vais et retourne à ma demeure, jusqu'à ce qu'ils se reconnaissent et cherchent ma face; dans leur angoisse ils voudront me trouver.