< Hosea 5 >

1 “Sikieni hili, enyi makuhani! Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli! Sikieni, ee nyumba ya mfalme! Hukumu hii ni dhidi yenu: Mmekuwa mtego huko Mispa, wavu uliotandwa juu ya Tabori.
« Écoutez ceci, vous, les prêtres! Écoutez, maison d'Israël, et écoutez, maison du roi! Car le jugement est contre vous; car tu as été un piège à Mitspa, et un écart net sur Tabor.
2 Waasi wamezidisha sana mauaji. Mimi nitawatiisha wote.
Les rebelles sont en plein massacre, mais je les discipline tous.
3 Ninajua yote kuhusu Efraimu, Israeli hukufichika kwangu. Efraimu, sasa umegeukia ukahaba, Israeli amenajisika.
Je connais Ephraïm, et Israël ne m'est pas caché; pour l'instant, Ephraim, tu as joué la prostituée. Israël est souillé.
4 “Matendo yao hayawaachii kurudi kwa Mungu wao. Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao, hawamkubali Bwana.
Leurs actes ne leur permettent pas de se tourner vers leur Dieu, car l'esprit de prostitution est en eux, et ils ne connaissent pas Yahvé.
5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao; Waisraeli, hata Efraimu, wanajikwaa katika dhambi zao; pia Yuda atajikwaa pamoja nao.
L'orgueil d'Israël témoigne de sa face. C'est pourquoi Israël et Ephraïm trébucheront dans leur iniquité. Juda aussi trébuchera avec eux.
6 Wakati wanapokwenda na makundi yao ya kondoo na ngʼombe kumtafuta Bwana, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.
Ils iront avec leurs troupeaux et leurs bêtes pour chercher Yahvé, mais ils ne le trouveront pas. Il s'est retiré d'eux.
7 Wao si waaminifu kwa Bwana; wamezaa watoto haramu. Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi zitawaangamiza wao pamoja na mashamba yao.
Ils sont infidèles à Yahvé; car elles ont porté des enfants illégitimes. Maintenant, la nouvelle lune va les dévorer avec leurs champs.
8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea, baragumu huko Rama. Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni, ongoza, ee Benyamini.
« Sonnez de la trompette à Gibéa, et la trompette à Rama! Sonnez un cri de guerre à Beth Aven, derrière vous, Benjamin!
9 Efraimu ataachwa ukiwa katika siku ya kuadhibiwa. Miongoni mwa makabila ya Israeli ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.
Ephraïm deviendra une désolation au jour du châtiment. Parmi les tribus d'Israël, j'ai fait connaître ce qui sera sûrement.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mawe ya mpaka. Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama mafuriko ya maji.
Les princes de Juda sont comme ceux qui enlèvent un repère. Je déverserai ma colère sur eux comme de l'eau.
11 Efraimu ameonewa, amekanyagwa katika hukumu kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.
Ephraïm est opprimé, il est écrasé par le jugement, parce qu'il est déterminé dans sa poursuite des idoles.
12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa watu wa Yuda.
C'est pourquoi je suis pour Éphraïm comme un papillon de nuit, et à la maison de Juda comme une pourriture.
13 “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake, naye Yuda vidonda vyake, ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru, na kuomba msaada kwa mfalme mkuu. Lakini hawezi kukuponya, wala hawezi kukuponya vidonda vyako.
« Quand Ephraïm vit sa maladie, et Juda sa blessure, puis Ephraïm est allé en Assyrie, et envoyé au roi Jareb: mais il n'est pas capable de vous guérir, il ne vous guérira pas non plus de votre blessure.
14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu, kama simba mkubwa kwa Yuda. Nitawararua vipande vipande na kuondoka; nitawachukua mbali, na hakuna wa kuwaokoa.
Car je serai pour Ephraïm comme un lion, et comme un jeune lion à la maison de Juda. Je vais moi-même me déchirer en morceaux et m'en aller. J'emporterai, et il n'y aura personne pour délivrer.
15 Kisha nitarudi mahali pangu mpaka watakapokubali kosa lao. Nao watautafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”
Je vais m'en aller et retourner à ma place, jusqu'à ce qu'ils reconnaissent leur offense, et cherchez ma face. Dans leur détresse, ils me chercheront avec ardeur. »

< Hosea 5 >