< Hosea 5 >
1 “Sikieni hili, enyi makuhani! Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli! Sikieni, ee nyumba ya mfalme! Hukumu hii ni dhidi yenu: Mmekuwa mtego huko Mispa, wavu uliotandwa juu ya Tabori.
“Hear this, priests! Pay attention, house of Israel! Listen, house of the king! For judgment is coming against you all. You have been a snare at Mizpah and a net spread over Tabor.
2 Waasi wamezidisha sana mauaji. Mimi nitawatiisha wote.
The rebels stand deep in slaughter, but I will punish all of them.
3 Ninajua yote kuhusu Efraimu, Israeli hukufichika kwangu. Efraimu, sasa umegeukia ukahaba, Israeli amenajisika.
I know Ephraim, and Israel is not hidden from me. Ephraim, now you have become like a prostitute; Israel is defiled.
4 “Matendo yao hayawaachii kurudi kwa Mungu wao. Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao, hawamkubali Bwana.
Their deeds will not allow them to turn to God, for the mind of adultery is in them, and they do not know Yahweh.
5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao; Waisraeli, hata Efraimu, wanajikwaa katika dhambi zao; pia Yuda atajikwaa pamoja nao.
The pride of Israel testifies against him; so Israel and Ephraim will stumble in their guilt; and Judah also will stumble with them.
6 Wakati wanapokwenda na makundi yao ya kondoo na ngʼombe kumtafuta Bwana, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.
They will go with their flocks and herds to seek Yahweh, but they will not find him, for he has withdrawn himself from them.
7 Wao si waaminifu kwa Bwana; wamezaa watoto haramu. Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi zitawaangamiza wao pamoja na mashamba yao.
They were unfaithful to Yahweh, for they have borne illegitimate children. Now the new moon festivals will devour them with their fields.
8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea, baragumu huko Rama. Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni, ongoza, ee Benyamini.
Blow the horn in Gibeah, and the trumpet in Ramah. Sound a battle cry at Beth Aven: 'We will follow you, Benjamin!'
9 Efraimu ataachwa ukiwa katika siku ya kuadhibiwa. Miongoni mwa makabila ya Israeli ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.
Ephraim will become a desolation on the day of punishment. Among the tribes of Israel I have declared what is certain to happen.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mawe ya mpaka. Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama mafuriko ya maji.
The leaders of Judah are like those who move a boundary stone. I will pour my wrath on them like water.
11 Efraimu ameonewa, amekanyagwa katika hukumu kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.
Ephraim is crushed; he is crushed in judgment, because he has willingly walked after idols.
12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa watu wa Yuda.
So I will be like a moth to Ephraim, and like rot to the house of Judah.
13 “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake, naye Yuda vidonda vyake, ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru, na kuomba msaada kwa mfalme mkuu. Lakini hawezi kukuponya, wala hawezi kukuponya vidonda vyako.
When Ephraim saw his sickness, and Judah saw his wound, then Ephraim went to Assyria, and Judah sent messengers to the great king. But he was not able to cure you people or heal your wound.
14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu, kama simba mkubwa kwa Yuda. Nitawararua vipande vipande na kuondoka; nitawachukua mbali, na hakuna wa kuwaokoa.
So I will be like a lion to Ephraim, and like a young lion to the house of Judah. I, even I, will tear and go away; I will carry them off, and there will be no one to rescue them.
15 Kisha nitarudi mahali pangu mpaka watakapokubali kosa lao. Nao watautafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”
I will go and return to my place, until they acknowledge their guilt and seek my face, until they earnestly seek me in their distress.”