< Hosea 5 >

1 “Sikieni hili, enyi makuhani! Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli! Sikieni, ee nyumba ya mfalme! Hukumu hii ni dhidi yenu: Mmekuwa mtego huko Mispa, wavu uliotandwa juu ya Tabori.
Hear ye this, O ye priests, And hearken, O house of Israel, And give ear, O house of the king! For judgment is coming upon you, Because ye have been a snare at Mizpah, And an outspread net upon Tabor.
2 Waasi wamezidisha sana mauaji. Mimi nitawatiisha wote.
By their sacrifices they commit deep transgression, And I will bring chastisement upon them all.
3 Ninajua yote kuhusu Efraimu, Israeli hukufichika kwangu. Efraimu, sasa umegeukia ukahaba, Israeli amenajisika.
I know Ephraim, And Israel is not hidden from me; For thou committest fornication, O Ephraim, And Israel is defiled.
4 “Matendo yao hayawaachii kurudi kwa Mungu wao. Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao, hawamkubali Bwana.
They will not frame their doings To return to their God; For a spirit of fornication is within them, And they have no regard to Jehovah.
5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao; Waisraeli, hata Efraimu, wanajikwaa katika dhambi zao; pia Yuda atajikwaa pamoja nao.
The pride of Israel testifieth to his face; Therefore shall Israel and Ephraim fall in their iniquity; Judah also shall fall with them.
6 Wakati wanapokwenda na makundi yao ya kondoo na ngʼombe kumtafuta Bwana, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.
With their flocks and with their herds shall they go to seek Jehovah, And shall not find him; He hath withdrawn himself from them.
7 Wao si waaminifu kwa Bwana; wamezaa watoto haramu. Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi zitawaangamiza wao pamoja na mashamba yao.
They have been false to Jehovah, For they have begotten strange children; Now shall the new moon consume them with their possessions.
8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea, baragumu huko Rama. Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni, ongoza, ee Benyamini.
Blow ye the trumpet in Gibeah, And the cornet in Ramah; Cry aloud at Bethaven! Look behind thee, O Benjamin!
9 Efraimu ataachwa ukiwa katika siku ya kuadhibiwa. Miongoni mwa makabila ya Israeli ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.
Ephraim shall be desolate in the day of rebuke; Among the tribes of Israel do I make known what is sure.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mawe ya mpaka. Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama mafuriko ya maji.
The princes of Judah are like them that remove the land mark; I will pour out my wrath upon them like water.
11 Efraimu ameonewa, amekanyagwa katika hukumu kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.
Ephraim is oppressed; he is crushed with punishment, Because he willingly walked after the decree.
12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa watu wa Yuda.
I am as a moth to Ephraim, And as rottenness to the house of Judah.
13 “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake, naye Yuda vidonda vyake, ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru, na kuomba msaada kwa mfalme mkuu. Lakini hawezi kukuponya, wala hawezi kukuponya vidonda vyako.
When Ephraim saw his sickness, And Judah his wound, Then went Ephraim to the Assyrian, And Judah sent to the hostile king; But he will not be able to heal you, Nor will he cure you of your wound.
14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu, kama simba mkubwa kwa Yuda. Nitawararua vipande vipande na kuondoka; nitawachukua mbali, na hakuna wa kuwaokoa.
For I will be as a lion to Ephraim, And as a young lion to the house of Judah. I, even I, will tear, and will depart; I will take away, and none shall rescue.
15 Kisha nitarudi mahali pangu mpaka watakapokubali kosa lao. Nao watautafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”
I will go back to my place, Till they have suffered for their sin, and seek my face! In their affliction they will seek me early.

< Hosea 5 >