< Hosea 5 >

1 “Sikieni hili, enyi makuhani! Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli! Sikieni, ee nyumba ya mfalme! Hukumu hii ni dhidi yenu: Mmekuwa mtego huko Mispa, wavu uliotandwa juu ya Tabori.
O ye Priestes, heare this, and hearken ye, O house of Israel, and giue ye eare, O house of the King: for iudgement is towarde you, because you haue bene a snare on Mizpah, and a net spred vpon Tabor.
2 Waasi wamezidisha sana mauaji. Mimi nitawatiisha wote.
Yet they were profounde, to decline to slaughter, though I haue bene a rebuker of them all.
3 Ninajua yote kuhusu Efraimu, Israeli hukufichika kwangu. Efraimu, sasa umegeukia ukahaba, Israeli amenajisika.
I knowe Ephraim, and Israel is not hid from me: for nowe, O Ephraim thou art become an harlot, and Israel is defiled.
4 “Matendo yao hayawaachii kurudi kwa Mungu wao. Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao, hawamkubali Bwana.
They will not giue their mindes to turne vnto their God: for the spirit of fornication is in the middes of them, and they haue not knowen the Lord.
5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao; Waisraeli, hata Efraimu, wanajikwaa katika dhambi zao; pia Yuda atajikwaa pamoja nao.
And the pride of Israel doth testifie to his face: therefore shall Israel and Ephraim fall in their iniquitie: Iudah also shall fall with them.
6 Wakati wanapokwenda na makundi yao ya kondoo na ngʼombe kumtafuta Bwana, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.
They shall goe with their sheepe, and with their bullockes to seeke the Lord: but they shall not finde him: for he hath withdrawne himselfe from them.
7 Wao si waaminifu kwa Bwana; wamezaa watoto haramu. Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi zitawaangamiza wao pamoja na mashamba yao.
They haue transgressed against the Lord: for they haue begotte strange children: now shall a moneth deuoure them with their portions.
8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea, baragumu huko Rama. Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni, ongoza, ee Benyamini.
Blowe ye the trumpet in Gibeah, and the shaume in Ramah: crie out at Beth-auen, after thee, O Beniamin.
9 Efraimu ataachwa ukiwa katika siku ya kuadhibiwa. Miongoni mwa makabila ya Israeli ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.
Ephraim shall be desolate in the day of rebuke: among the tribes of Israel haue I caused to knowe the trueth.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mawe ya mpaka. Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama mafuriko ya maji.
The princes of Iudah were like them that remoue the bounde: therefore will I powre out my wrath vpon them like water.
11 Efraimu ameonewa, amekanyagwa katika hukumu kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.
Ephraim is oppressed, and broken in iudgement, because he willingly walked after the commandement.
12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa watu wa Yuda.
Therefore wil I be vnto Ephraim as a moth, and to the house of Iudah as a rottennesse.
13 “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake, naye Yuda vidonda vyake, ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru, na kuomba msaada kwa mfalme mkuu. Lakini hawezi kukuponya, wala hawezi kukuponya vidonda vyako.
When Ephraim sawe his sickenes, and Iudah his wound, then went Ephraim vnto Asshur, and sent vnto King Iareb: yet coulde hee not heale you, nor cure you of your wound.
14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu, kama simba mkubwa kwa Yuda. Nitawararua vipande vipande na kuondoka; nitawachukua mbali, na hakuna wa kuwaokoa.
For I will be vnto Ephraim as a lyon, and as a lyons whelpe to the house of Iudah: I, euen I will spoyle, and goe away: I will take away, and none shall rescue it.
15 Kisha nitarudi mahali pangu mpaka watakapokubali kosa lao. Nao watautafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”
I will go, and returne to my place, til they acknowledge their fault, and seeke me: in their affliction they will seeke me diligently.

< Hosea 5 >