< Hosea 4 >

1 Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli, kwa sababu Bwana analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
Escuchen la palabra de Yahvé, hijos de Israel, porque Yahvé tiene una acusación contra los habitantes de la tierra: “En efecto, no hay verdad, ni bondad, ni el conocimiento de Dios en la tierra.
2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
Hay maldiciones, mentiras, asesinatos, robos y adulterios; rompen los límites, y el derramamiento de sangre provoca el derramamiento de sangre.
3 Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote waishio ndani mwake wanadhoofika, wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
Por lo tanto, la tierra estará de luto, y todo el que habite en ella se consumirá, con todos los seres vivos en ella, incluso los animales del campo y las aves del cielo; Sí, los peces del mar también mueren.
4 “Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
“Pero que nadie presente una acusación, ni que nadie acuse; porque tu pueblo es como los que acusan a un sacerdote.
5 Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
En el día tropezarás, y el profeta también tropezará contigo en la noche; y destruiré a tu madre.
6 watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
Mi pueblo es destruido por falta de conocimiento. Porque has rechazado el conocimiento, yo también te rechazaré, para que no seas un sacerdote para mí. Porque has olvidado la ley de tu Dios, También olvidaré a sus hijos.
7 Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
Como se multiplicaron, así pecaron contra mí. Cambiaré su gloria en vergüenza.
8 Hujilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
Se alimentan del pecado de mi pueblo, y ponen su corazón en su iniquidad.
9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
Será como la gente, como el sacerdote; y los castigaré por sus caminos, y les pagará por sus actos.
10 “Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Bwana na kujiingiza wenyewe
Comerán y no tendrán suficiente. Harán de prostituta, y no aumentarán; porque han dejado de escuchar a Yahvé.
11 katika ukahaba, divai ya zamani na divai mpya, ambavyo huondoa ufahamu
La prostitución, el vino y el vino nuevo quitan el entendimiento.
12 wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
Mi pueblo consulta con su ídolo de madera, y responder a un palo de madera. En efecto, el espíritu de la prostitución les ha llevado por el mal camino, y han sido infieles a su Dios.
13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
Sacrifican en las cimas de las montañas, y quemar incienso en las colinas, bajo las encinas, los álamos y los terebintales, porque su sombra es buena. Por lo tanto, sus hijas hacen el papel de prostituta, y tus novias cometen adulterio.
14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa kuabudia miungu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
No castigaré a tus hijas cuando jueguen a la prostitución, ni a sus novias cuando cometen adulterio; porque los hombres se prostituyen, y sacrifican con las prostitutas del santuario; por lo que la gente sin entendimiento llegará a la ruina.
15 “Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni Wala usiape, ‘Hakika kama Bwana aishivyo!’
“Aunque tú, Israel, te hagas la prostituta, pero no dejes que Judá se ofenda; y no vengas a Gilgal, ni subir a Beth Aven, ni jurar: “Vive Yahvé”.
16 Waisraeli ni wakaidi, kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi. Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
Porque Israel se ha comportado con extrema terquedad, como una vaquilla obstinada. Entonces, ¿cómo los alimentará Yahvé como a un cordero en un prado?
17 Efraimu amejiunga na sanamu, ondokana naye!
Efraín está unido a los ídolos. ¡Déjalo en paz!
18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
Su bebida se ha agriado. Hacen el papel de prostituta continuamente. Sus gobernantes aman su vergonzoso camino.
19 Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.
El viento la ha envuelto en sus alas; y se verán defraudados a causa de sus sacrificios.

< Hosea 4 >