< Hosea 4 >
1 Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli, kwa sababu Bwana analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
Poslušajte Gospodovo besedo, vi Izraelovi otroci, kajti Gospod ima polemiko s prebivalci dežele, zato ker tam ni resnice niti usmiljenja niti spoznanja Boga v deželi.
2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
S priseganjem, laganjem, ubijanjem, krajo in zagrešitvami zakonolomstva so izbruhnili in kri se dotika krvi.
3 Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote waishio ndani mwake wanadhoofika, wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
Zato bo dežela žalovala in kdor v njej prebiva bo opešal, z živalmi polja in s perjadjo neba. Da, tudi ribe morja bodo odvzete.
4 “Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
Vendarle naj se noben človek ne prepira niti naj ne graja drugega, kajti tvoje ljudstvo je kakor tisti, ki se prepirajo z duhovnikom.
5 Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
»Zato boš padel podnevi in tudi prerok bo padel s teboj ponoči in jaz bom uničil tvojo mater.
6 watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
Moje ljudstvo je uničeno zaradi pomanjkanja spoznanja. Ker si zavrnil spoznanje, bom tudi jaz zavrnil tebe, da mi ne boš duhovnik. Ker si pozabil postavo svojega Boga, bom tudi jaz pozabil tvoje otroke.
7 Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
Kakor so bili pomnoženi, tako so grešili zoper mene, zato bom njihovo slavo spremenil v sramoto.
8 Hujilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
Jedo greh mojega ljudstva in svoja srca naravnavajo na svojo krivičnost.
9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
In tam bo, kakršno ljudstvo, takšen duhovnik, in jaz jih bom kaznoval za njihove poti in jim nagradil njihova početja.
10 “Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Bwana na kujiingiza wenyewe
Kajti jedli bodo, pa ne bodo imeli dovolj, zagrešili bodo vlačugarstvo, pa se ne bodo pomnožili, ker so opustili, da bi bili pozorni na Gospoda.
11 katika ukahaba, divai ya zamani na divai mpya, ambavyo huondoa ufahamu
Vlačugarstvo, vino in novo vino jemljejo srce.
12 wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
Moje ljudstvo sprašuje za nasvet pri svojih kladah in njihova palica jim napoveduje, kajti duh vlačugarstev jim je povzročil, da blodijo in odšli so se vlačugat proč izpred svojega Boga.
13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
Žrtvujejo na vrhovih gora in kadilo zažigajo na hribih, pod hrasti, topoli in bresti, ker je njihova senca dobra. Zatorej bodo vaše hčere zagrešile vlačugarstvo in vaše snahe bodo zagrešile zakonolomstvo.
14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa kuabudia miungu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
Ne bom kaznoval vaših hčera, ko bodo zagrešile vlačuganje niti vaših snah, kadar bodo zagrešile zakonolomstvo, kajti oni sami so oddvojeni z vlačugami in žrtvujejo s pocestnicami. Zatorej bo ljudstvo, ki ne razume, padlo.
15 “Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni Wala usiape, ‘Hakika kama Bwana aishivyo!’
Čeprav ti, Izrael, igraš pocestnico, naj vendar Juda ne greši. Ne prihajajte v Gilgál, niti ne hodite gor v Bet Aven, niti ne prisegajte: › Gospod živi.‹
16 Waisraeli ni wakaidi, kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi. Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
Kajti Izrael drsi nazaj kakor nazaj zdrknjena telica. Sedaj jih bo Gospod pasel kakor jagnje na velikem kraju.
17 Efraimu amejiunga na sanamu, ondokana naye!
Efrájim je pridružen malikom, pusti ga samega.
18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
Njihova pijača je kisla. Spet in spet zagrešujejo vlačugarstvo. Njegovi vladarji ljubijo s sramoto: ›Dajajte.‹
19 Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.
Veter je [Izraela] zvezal v svoje peruti in osramočeni bodo zaradi svojih [klavnih] daritev.