< Hosea 4 >
1 Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli, kwa sababu Bwana analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
Hear the word of Yahweh, you people of Israel. Yahweh has a lawsuit against the inhabitants of the land, because there is no truthfulness or covenantal faithfulness, no knowledge of God in the land.
2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
There is cursing, lying, killing, stealing and adultery. The people have broken all bounds, and bloodshed comes after bloodshed.
3 Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote waishio ndani mwake wanadhoofika, wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
So the land is drying up, and everyone living in it is wasting away; the beasts in the fields and the birds in the sky, even the fish in the sea, are being taken away.
4 “Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
But do not allow anyone to bring a lawsuit; do not let anyone accuse anyone else. For it is you, the priests, whom I am accusing.
5 Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
You priests will stumble during the day; the prophets will also stumble with you by night, and I will destroy your mother.
6 watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
My people are being destroyed because of the lack of knowledge. Because you priests have rejected knowledge, I will also reject you as priests to me. Because you have forgotten my law, although I am your God, I also will forget your children.
7 Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
The more the priests multiplied, the more they sinned against me. They exchanged their honor for shame.
8 Hujilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
They feed on the sin of my people; they are greedy for more of their wickedness.
9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
It will be the same for the people as for the priests: I will punish them all for their practices; I will repay them for their deeds.
10 “Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Bwana na kujiingiza wenyewe
They will eat but not have enough; they will commit prostitution but not increase, because they have gone far away from Yahweh.
11 katika ukahaba, divai ya zamani na divai mpya, ambavyo huondoa ufahamu
They love sexual promiscuity, wine, and new wine, which have taken away their understanding.
12 wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
My people consult their wooden idols, and their walking sticks give them prophecies. For a mind of promiscuity has misled them, and they have acted as prostitutes instead of being faithful to their God.
13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
They sacrifice on the tops of the mountains and burn incense on the hills, under oaks, poplars and terebinths, because the shade is good. So your daughters commit sexual immorality, and your daughters-in-law commit adultery.
14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa kuabudia miungu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
I will not punish your daughters when they choose to commit sexual immorality, nor your daughters-in-law when they commit adultery. For the men also give themselves to the prostitutes, and they offer sacrifices so they can commit immoral acts with sacred prostitutes. So this people who does not understand will be thrown down.
15 “Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni Wala usiape, ‘Hakika kama Bwana aishivyo!’
Though you, Israel, have committed adultery, may Judah not become guilty. Do not go to Gilgal, you people; do not go up to Beth Aven, and do not swear, saying, “As Yahweh lives.”
16 Waisraeli ni wakaidi, kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi. Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
For Israel has behaved stubbornly, like a stubborn heifer. How can Yahweh bring them to pasture like lambs in a meadow?
17 Efraimu amejiunga na sanamu, ondokana naye!
Ephraim united himself with idols; leave him alone.
18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
Even when their strong drink is gone, they continue to commit adultery; her rulers dearly love their shame.
19 Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.
The wind will wrap her up in its wings; and they will be ashamed because of their sacrifices.