< Hosea 4 >

1 Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli, kwa sababu Bwana analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
Heare the worde of the Lord, ye children of Israel: for the Lord hath a controuersie with the inhabitants of the lande, because there is no trueth nor mercie nor knowledge of God in the lande.
2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
By swearing, and lying, and killing, and stealing, and whoring they breake out, and blood toucheth blood.
3 Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote waishio ndani mwake wanadhoofika, wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
Therefore shall the land mourne, and euery one that dwelleth therein, shall be cut off, with the beasts of the fielde, and with the foules of the heauen, and also the fishes of the sea shall be taken away.
4 “Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
Yet let none rebuke, nor reproue another: for thy people are as they that rebuke the Priest.
5 Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
Therefore shalt thou fall in the day, and the Prophet shall fall with thee in the night, and I will destroy thy mother.
6 watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
My people are destroyed for lacke of knowledge: because thou hast refused knowledge, I will also refuse thee, that thou shalt be no Priest to me: and seeing thou hast forgotten the Lawe of thy God, I will also forget thy children.
7 Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
As they were increased, so they sinned against me: therefore will I chaunge their glorie into shame.
8 Hujilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
They eate vp the sinnes of my people, and lift vp their mindes in their iniquitie.
9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
And there shalbe like people, like Priest: for I wil visite their wayes vpon them, and reward them their deedes.
10 “Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Bwana na kujiingiza wenyewe
For they shall eate, and not haue ynough: they shall commit adulterie, and shall not increase, because they haue left off to take heede to ye Lord.
11 katika ukahaba, divai ya zamani na divai mpya, ambavyo huondoa ufahamu
Whoredome, and wine, and newe wine take away their heart.
12 wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
My people aske counsell at their stockes, and their staffe teacheth them: for the spirite of fornications hath caused them to erre, and they haue gone a whoring from vnder their God.
13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
They sacrifice vpon the toppes of ye mountaines, and burne incense vpon the hilles vnder the okes, and the poplar tree, and the elme, because the shadow thereof is good: therefore your daughters shall be harlots, and your spouses shall be whores.
14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa kuabudia miungu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
I will not visite your daughters when they are harlots: nor your spouses when they are whores: for they themselues are separated with harlots, and sacrifice with whores: therefore the people that doeth not vnderstand, shall fall.
15 “Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni Wala usiape, ‘Hakika kama Bwana aishivyo!’
Though thou, Israel, play the harlot, yet let not Iudah sinne: come not ye vnto Gilgal, neither goe ye vp to Beth-auen, nor sweare, The Lord liueth.
16 Waisraeli ni wakaidi, kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi. Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
For Israel is rebellious as an vnruly heyfer. Nowe the Lord will feede them as a lambe in a large place.
17 Efraimu amejiunga na sanamu, ondokana naye!
Ephraim is ioyned to idoles: let him alone.
18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
Their drunkennes stinketh: they haue committed whoredome: their rulers loue to say with shame, Bring ye.
19 Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.
The winde hath bounde them vp in her wings, and they shalbe ashamed of their sacrifices.

< Hosea 4 >