< Hosea 4 >

1 Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli, kwa sababu Bwana analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
Listen to the word of the Lord, sons of Israel, for the Lord is judge of the inhabitants of the land. Yet there is no truth, and there is no mercy, and there is no knowledge of God, in the land.
2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
Slander, and lying, and killing, and theft, and adultery have overflowed, and bloodshed has brought more bloodshed.
3 Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote waishio ndani mwake wanadhoofika, wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
Because of this, the land will mourn, and all who dwell in it will languish, with the beasts of the field and the birds of the air. And the fishes of the sea also will be gathered together.
4 “Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
So, truly, let each and every one not judge, and let no man be accused, for your people are just like those who speak against the priesthood.
5 Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
And you will be ruined on this day, and now the prophet will be ruined with you. In the night, I have made your mother to be silent.
6 watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
My people have become silent because they had no knowledge. Since you have rejected knowledge, I will drive you away; you do not perform the duties of the priesthood for me, and you have forgotten the law of your God, and so I will forget your sons.
7 Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
According to the multitude of them, so have they sinned against me. I will change their glory into disgrace.
8 Hujilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
They will devour the sins of my people, and they will lift up their souls towards their iniquity.
9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
And, just as it is with the people, so will it be with the priest; and I will visit their ways upon them, and I will repay them for their intentions.
10 “Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Bwana na kujiingiza wenyewe
And they will eat and not be satisfied. They have been committing fornication, and they did not cease. Since they have abandoned the Lord, they will not be safeguarded.
11 katika ukahaba, divai ya zamani na divai mpya, ambavyo huondoa ufahamu
Fornication, and wine, and drunkenness, have taken away their heart.
12 wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
My people have inquired of their stave, and their staff has announced to them. For the spirit of fornication has deceived them, and they have been fornicating before their God.
13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
They have offered sacrifice on the tops of the mountains and burnt incense on the hills, under the oak, and the poplar, and the terebinth tree, because its shadow was good; therefore, your daughters will commit fornication and your spouses will be adulteresses.
14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa kuabudia miungu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
I will not send afflictions on your daughters, when they will commit fornication, nor on your spouses, when they will commit adultery, because you yourselves have associated with harlots and have offered sacrifice with the effeminate, and because the people who do not understand will be defeated.
15 “Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni Wala usiape, ‘Hakika kama Bwana aishivyo!’
If you commit fornication, Israel, at least let Judah not commit offenses; and do not be willing to enter into Gilgal, nor to ascend to Bethaven, and neither should you swear, “As the Lord lives.”
16 Waisraeli ni wakaidi, kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi. Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
For Israel has gone astray like a wanton heifer; so now the Lord will pasture them like a young lamb in a wide expanse.
17 Efraimu amejiunga na sanamu, ondokana naye!
Ephraim participates in idolatry, so send him away.
18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
Their feasting has been set aside; they have committed fornication after fornication. They love to bring disgrace to their protectors.
19 Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.
The wind has fastened them to its wings, and they will be confounded because of their sacrifices.

< Hosea 4 >