< Hosea 2 >

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
Appelez vos frères Hammi, et vos sœurs Ruhama.
2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni, kwa maana yeye si mke wangu, nami si mume wake. Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake na uzinzi kati ya matiti yake.
Plaidez, plaidez avec votre mère, car elle n'[est] point ma femme, et aussi ne suis-je point son mari; et qu'elle ôte ses prostitutions de devant elle, et ses adultères de son sein.
3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa. Nitamfanya kama jangwa, nitamgeuza awe nchi ya kiu, nami nitamuua kwa kiu.
De peur que je ne manifeste sa nudité, que je ne la remette dans l'état où elle était le jour qu'elle naquit, que je ne la réduise en désert, et que je ne la fasse être comme une terre sèche, et ne la fasse mourir de soif.
4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake, kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
Et que je n'use point de miséricorde envers ses enfants, car ce sont des enfants de prostitution.
5 Mama yao amekosa uaminifu na amewachukua mimba katika aibu. Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu, ambao hunipa chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
Parce que leur mère s'est prostituée, celle qui les a conçus s'est déshonorée, car elle a dit: Je m'en irai après ceux que j'aime, qui me donnent mon pain et mes eaux, ma laine, et mon lin, mon huile, et mes boissons.
6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake kwa vichaka vya miiba, nitamjengea ukuta ili kwamba asiweze kutoka.
C'est pourquoi, voici, je boucherai d'épines ton chemin, et je ferai une cloison de pierres, en sorte qu'elle ne trouvera point ses sentiers.
7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata; atawatafuta lakini hatawapata. Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza, kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi kuliko sasa.’
Elle ira donc vers ceux dont elle recherche l'amitié; mais elle ne les atteindra point; elle les cherchera, mais elle ne les trouvera point; et elle dira: Je m'en irai et retournerai à mon premier mari, car alors j'étais mieux que je ne suis maintenant.
8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta, niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia kwa kumtumikia Baali.
Mais elle n'a point connu que c'était moi qui lui avais donné le froment, et le vin, et l'huile, et qui lui avais multiplié l'argent et l'or dont ils ont fait un Bahal.
9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari. Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
C'est pourquoi je viendrai à reprendre mon froment en son temps, et mon vin en sa saison, et je retirerai ma laine et mon lin qui couvraient sa nudité.
10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake mbele ya wapenzi wake; hakuna yeyote atakayemtoa mikononi mwangu.
Et maintenant je découvrirai sa turpitude devant les yeux de ceux qui l'aiment, et personne ne la délivrera de ma main.
11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote: sikukuu zake za mwaka, sikukuu za Miandamo ya Mwezi, siku zake za Sabato, sikukuu zake zote zilizoamriwa.
Je ferai cesser toute sa joie, ses fêtes, ses nouvelles lunes, ses Sabbats, et toutes ses solennités.
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema yalikuwa malipo yake kutoka kwa wapenzi wake; nitaifanya kuwa kichaka, nao wanyama pori wataila.
Et je gâterai ses vignobles, et ses figuiers, desquels elle a dit: Ce sont ici mes salaires que ceux qui m'aiment m'ont donnés; et je les réduirai en forêt, et les bêtes des champs les dévoreront.
13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku alizowafukizia uvumba Mabaali; alipojipamba kwa pete na kwa vito vya thamani, na kuwaendea wapenzi wake, lakini mimi alinisahau,” asema Bwana.
Et je visiterai sur elle les jours des Bahalins, durant lesquels elle leur faisait des parfums, et se parait de ses bagues et de ses joyaux, et s'en allait après ceux qui l'aimaient, et m'oubliait, dit l'Eternel.
14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi; nitamwongoza hadi jangwani na kuzungumza naye kwa upole.
Néanmoins, voici, je l'attirerai après que je l'aurai promenée par le désert, et je lui parlerai selon son cœur.
15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu, nami nitalifanya Bonde la Akori mlango wa matumaini. Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama siku zile alizotoka Misri.
Et je lui donnerai ses vignes, depuis ce lieu-là, et la vallée de Hachor, pour l'entrée de son attente, et elle y chantera comme au temps de sa jeunesse, et comme lorsqu'elle remonta du pays d'Egypte.
16 “Katika siku ile,” asema Bwana, “utaniita mimi ‘Mume wangu’; hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
Et il arrivera en ce jour-là, dit l'Eternel, que tu m'appelleras, Mon mari, et que tu ne m'appelleras plus, Mon Bahal.
17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake, wala hataomba tena kwa majina yao.
Car j'ôterai de sa bouche les noms des Bahalins, et on n'en fera plus mention par leur nom.
18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani, na viumbe vile vitambaavyo ardhini. Upinde, upanga na vita, nitaondolea mbali katika nchi, ili kwamba wote waweze kukaa salama.
Aussi en ce temps-là je traiterai pour eux une alliance avec les bêtes des champs, et avec les oiseaux des cieux, et avec les reptiles de la terre; et je briserai [et j'ôterai] du pays, l'arc, et l'épée, et la guerre, et je les ferai dormir en sûreté.
19 Nitakuposa uwe wangu milele; nitakuposa kwa uadilifu na haki, kwa upendo na huruma.
Et je t'épouserai pour moi à toujours; je t'épouserai, dis-je, pour moi, en justice, et en jugement, et en gratuité, et en compassions.
20 Nitakuposa kwa uaminifu, nawe utamkubali Bwana.
Même je t'épouserai en fermeté, et tu connaîtras l'Eternel.
21 “Katika siku ile nitajibu,” asema Bwana, “nitajibu kwa anga, nazo anga zitajibu kwa nchi;
Et il arrivera en ce temps-là que je répondrai, dit l'Eternel, que je répondrai aux cieux, et les cieux répondront à la terre.
22 nayo nchi itajibu kwa nafaka, divai mpya na mafuta, navyo vitajibu kwa Yezreeli.
Et la terre répondra au froment, au bon vin, et à l'huile; et eux répondront à Jizréhel.
23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitaonyesha pendo langu kwake yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’ Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’ ‘Ninyi ni watu wangu’; nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’”
Puis je la sèmerai pour moi en la terre, et je ferai miséricorde à Lo-ruhama; et je dirai à Lo-hammi, tu es mon peuple; et il me dira, mon Dieu.

< Hosea 2 >