< Hosea 2 >

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
Dites à votre frère, Mon-Peuple, et à votre sœur Pitié:
2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni, kwa maana yeye si mke wangu, nami si mume wake. Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake na uzinzi kati ya matiti yake.
Plaidez contre votre mère; car elle n'est point Ma femme, et Je ne suis point son Mari. Et J'ôterai de devant Ma face sa prostitution, et son adultère du milieu de ses mamelles,
3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa. Nitamfanya kama jangwa, nitamgeuza awe nchi ya kiu, nami nitamuua kwa kiu.
afin de la mettre nue, et de la remettre comme elle était le jour de sa naissance; et Je ferai d'elle un désert, et Je la traiterai comme une terre aride; et Je la tuerai par la soif;
4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake, kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
et Je n'aurai point pitié de ses enfants; car ce sont des enfants de prostitution.
5 Mama yao amekosa uaminifu na amewachukua mimba katika aibu. Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu, ambao hunipa chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
Leur mère s'est prostituée; celle qui les a portés les a couverts de honte; elle a dit: Je m'en irai après mes amants qui me donnent mon pain, et mon eau, et mes vêtements, et mon linge, et mon huile, et tout ce qui m'est nécessaire.
6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake kwa vichaka vya miiba, nitamjengea ukuta ili kwamba asiweze kutoka.
C'est pourquoi Je ferme sa voie avec des épines, et Je bâtirai sur ses routes; elle ne retrouvera plus son sentier.
7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata; atawatafuta lakini hatawapata. Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza, kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi kuliko sasa.’
Elle poursuivra ses amants, et ne les atteindra pas; elle les cherchera, et ne les trouvera pas; Et elle dira: Je vais partir, je vais retourner auprès de mon premier mari; car, pour moi, il faisait meilleur alors que maintenant.
8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta, niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia kwa kumtumikia Baali.
Et elle n'a point connu que Je lui avais donné du pain, du vin et de l'huile, et que Je l'avais comblée d'argent, et elle a fait à Baal des idoles d'argent et d'or.
9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari. Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
À cause de cela, Je M'en retournerai, Je prendrai Mon blé lors de la moisson, et Mon vin lors de la vendange; et Je reprendrai Mes vêtements et Mon linge, pour ne plus couvrir sa nudité.
10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake mbele ya wapenzi wake; hakuna yeyote atakayemtoa mikononi mwangu.
Et désormais Je révélerai à ses amants son impureté, et nul ne la délivrera de Mes mains.
11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote: sikukuu zake za mwaka, sikukuu za Miandamo ya Mwezi, siku zake za Sabato, sikukuu zake zote zilizoamriwa.
Et Je supprimerai toutes ses joies, toutes ses fêtes, toutes ses nouvelles lunes, ses sabbats et toutes ses solennités.
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema yalikuwa malipo yake kutoka kwa wapenzi wake; nitaifanya kuwa kichaka, nao wanyama pori wataila.
Et Je détruirai sa vigne et ses figuiers, parce qu'elle a dit: Ce sont les salaires que m'ont donné mes amants. Et Moi, J'en ferai un témoignage; les bêtes des champs viendront y paître, et les oiseaux du ciel, et les reptiles de la terre.
13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku alizowafukizia uvumba Mabaali; alipojipamba kwa pete na kwa vito vya thamani, na kuwaendea wapenzi wake, lakini mimi alinisahau,” asema Bwana.
Je lui ferai expier les jours où elle a sacrifié à Baal, et où elle a mis ses pendants d'oreilles et ses colliers pour s'en aller après son amant. Et elle M'a oublié, dit le Seigneur.
14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi; nitamwongoza hadi jangwani na kuzungumza naye kwa upole.
C'est pourquoi Je l'égarerai et Je l'enverrai dans le désert, et je parlerai à son cœur.
15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu, nami nitalifanya Bonde la Akori mlango wa matumaini. Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama siku zile alizotoka Misri.
Et de là Je lui rendrai ses possessions et la vallée d'Achor, pour lui ouvrir l'intelligence. Et là elle s'humiliera autant de jours qu'a duré sa jeunesse, et autant de jours qu'elle a mis à revenir de la terre d'Égypte.
16 “Katika siku ile,” asema Bwana, “utaniita mimi ‘Mume wangu’; hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
Et ceci arrivera en ce jour-là, dit le Seigneur; elle M'appellera Mon époux, et elle ne M'appellera plus Baal.
17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake, wala hataomba tena kwa majina yao.
Et J'ôterai de sa bouche les noms de Baal, et l'on ne s'en souviendra plus.
18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani, na viumbe vile vitambaavyo ardhini. Upinde, upanga na vita, nitaondolea mbali katika nchi, ili kwamba wote waweze kukaa salama.
Et en ce jour-là J'établirai une alliance entre eux et les bêtes sauvages, et les oiseaux du ciel, et les reptiles de la terre; et Je briserai sur la terre l'arc, le glaive et les armes de guerre, et Je t'y installerai avec l'espérance.
19 Nitakuposa uwe wangu milele; nitakuposa kwa uadilifu na haki, kwa upendo na huruma.
Et Je te prendrai pour épouse dans tous les siècles, et Je te prendrai pour épouse en Mon équité, en Mes jugements, en Ma pitié, en Ma miséricorde.
20 Nitakuposa kwa uaminifu, nawe utamkubali Bwana.
Et Je te prendrai pour épouse avec confiance, et tu reconnaîtras le Seigneur.
21 “Katika siku ile nitajibu,” asema Bwana, “nitajibu kwa anga, nazo anga zitajibu kwa nchi;
Et il arrivera en ce jour-là, dit le Seigneur, que J'exaucerai le ciel, et le ciel exaucera la terre.
22 nayo nchi itajibu kwa nafaka, divai mpya na mafuta, navyo vitajibu kwa Yezreeli.
Et la terre exaucera le blé, et le vin, et l'huile, et toutes ces choses exauceront Jezraël.
23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitaonyesha pendo langu kwake yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’ Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’ ‘Ninyi ni watu wangu’; nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’”
Et Je la sèmerai pour moi sur la terre, et J'aimerai celle que Je n'aimais pas. Et Je dirai à Non-Mon-Peuple: Tu es Mon peuple; et il dira: Tu es le Seigneur mon Dieu.

< Hosea 2 >