< Hosea 2 >

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
Dites à vos frères: " Ammi! " et à vos sœurs: " Ruchama! "
2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni, kwa maana yeye si mke wangu, nami si mume wake. Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake na uzinzi kati ya matiti yake.
Plaidez contre votre mère, plaidez! car elle n'est plus ma femme, et moi je ne suis plus son mari. Qu'elle éloigne de sa face ses prostitutions, et ses adultères du milieu de ses seins,
3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa. Nitamfanya kama jangwa, nitamgeuza awe nchi ya kiu, nami nitamuua kwa kiu.
de peur que je ne la déshabille à nu, et que je ne la mette telle qu'au jour de sa naissance, que je ne la rende pareille au désert, faisant d'elle une terre desséchée, et que je ne la fasse mourir de soif.
4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake, kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
Je n'aurai pas compassion de ses enfants, car ce sont des enfants de prostitution.
5 Mama yao amekosa uaminifu na amewachukua mimba katika aibu. Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu, ambao hunipa chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
Car leur mère s'est prostituée, celle qui les a conçus a fait des choses honteuses; elle a dit: " J'irai après mes amants, qui me donnent mon pain et mon eau, ma laine et mon lin, mon huile et ma boisson. "
6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake kwa vichaka vya miiba, nitamjengea ukuta ili kwamba asiweze kutoka.
C'est pourquoi voici que je vais fermer ton chemin avec des ronces; j'élèverai un mur, et elle ne trouvera plus ses sentiers.
7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata; atawatafuta lakini hatawapata. Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza, kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi kuliko sasa.’
Elle poursuivra ses amants et ne les atteindra pas; elle les cherchera et ne les trouvera pas. Puis elle dira: " J'irai et je retournerai vers mon premier mari, car j'étais plus heureuse alors que maintenant. "
8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta, niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia kwa kumtumikia Baali.
Elle n'a pas reconnu que c'est moi qui lui ai donné le froment, le vin nouveau et l'huile, qui lui ai multiplié l'argent et l'or, qu'ils ont employés pour Baal.
9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari. Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
C'est pourquoi je reprendrai mon froment en son temps, et mon vin nouveau dans sa saison, et je retirerai ma laine et mon lin, qui servent à couvrir sa nudité.
10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake mbele ya wapenzi wake; hakuna yeyote atakayemtoa mikononi mwangu.
Et maintenant je découvrirai sa honte, aux yeux de ses amants, et personne ne la dégagera de ma main.
11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote: sikukuu zake za mwaka, sikukuu za Miandamo ya Mwezi, siku zake za Sabato, sikukuu zake zote zilizoamriwa.
Je ferai cesser toutes ses réjouissances, ses fêtes, ses nouvelles lunes, ses sabbats, et toutes ses solennités.
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema yalikuwa malipo yake kutoka kwa wapenzi wake; nitaifanya kuwa kichaka, nao wanyama pori wataila.
Je dévasterai ses vignes et ses figuiers dont elle disait: " C'est le salaire que m'ont donné mes amants; " et je les réduirai en forêts, et les bêtes sauvages les dévoreront.
13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku alizowafukizia uvumba Mabaali; alipojipamba kwa pete na kwa vito vya thamani, na kuwaendea wapenzi wake, lakini mimi alinisahau,” asema Bwana.
Je la punirai pour les jours des Baals; auxquels elle offrait de l'encens; alors qu'elle se parait de son anneau et de son collier et allait après ses amants; et moi, elle m'oubliait, — oracle de Yahweh.
14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi; nitamwongoza hadi jangwani na kuzungumza naye kwa upole.
C'est pourquoi, voici que moi je l'attirerai, et la conduirai au désert, et je lui parlerai au cœur;
15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu, nami nitalifanya Bonde la Akori mlango wa matumaini. Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama siku zile alizotoka Misri.
et de là je lui donnerai ses vignes, et la vallée d'Achor comme une porte d'espérance; et elle répondra là comme aux jours de sa jeunesse, et comme au jour où elle monta hors du pays d'Egypte.
16 “Katika siku ile,” asema Bwana, “utaniita mimi ‘Mume wangu’; hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
En ce jour-là, — oracle de Yahweh, tu m'appelleras: " Mon mari ", et tu ne m'appelleras plus: " Mon Baal ".
17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake, wala hataomba tena kwa majina yao.
J'ôterai de sa bouche les noms des Baals, et ils ne seront plus mentionnés par leur nom.
18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani, na viumbe vile vitambaavyo ardhini. Upinde, upanga na vita, nitaondolea mbali katika nchi, ili kwamba wote waweze kukaa salama.
Je ferai pour eux un pacte, en ce jour, avec les bêtes sauvages, avec les oiseaux du ciel, et les reptiles de la terre; je ferai disparaître du pays l'arc, l'épée et la guerre, et je les ferai reposer en sécurité.
19 Nitakuposa uwe wangu milele; nitakuposa kwa uadilifu na haki, kwa upendo na huruma.
Je te fiancerai à moi pour toujours; je te fiancerai à moi dans la justice et le jugement, dans la grâce et la tendresse;
20 Nitakuposa kwa uaminifu, nawe utamkubali Bwana.
je te fiancerai à moi dans la fidélité, et tu connaîtras Yahweh.
21 “Katika siku ile nitajibu,” asema Bwana, “nitajibu kwa anga, nazo anga zitajibu kwa nchi;
Et il arrivera en ce jour, je répondrai, — oracle de Yahweh, je répondrai aux cieux, et eux répondront à la terre;
22 nayo nchi itajibu kwa nafaka, divai mpya na mafuta, navyo vitajibu kwa Yezreeli.
la terre répondra au froment, au vin nouveau et à l'huile, et eux répondront à Jezrahel.
23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitaonyesha pendo langu kwake yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’ Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’ ‘Ninyi ni watu wangu’; nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’”
J'ensemencerai pour moi Israël dans le pays, et je ferai miséricorde à Lô-Ruchama; je dirai à Lô-Ammi: " Tu es mon peuple! " et il dira: " Mon Dieu! "

< Hosea 2 >