< Hosea 2 >

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
to say to/for brother: compatriot your people my and to/for sister your to have compassion
2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni, kwa maana yeye si mke wangu, nami si mume wake. Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake na uzinzi kati ya matiti yake.
to contend in/on/with mother your to contend for he/she/it not woman: wife my and I not man: husband her and to turn aside: remove fornication her from face her and adultery her from between breast her
3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa. Nitamfanya kama jangwa, nitamgeuza awe nchi ya kiu, nami nitamuua kwa kiu.
lest to strip her naked and to set her like/as day to beget she and to set: make her like/as wilderness and to set: make her like/as land: country/planet dryness and to die her in/on/with thirst
4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake, kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
and [obj] son: child her not to have compassion for son: child fornication they(masc.)
5 Mama yao amekosa uaminifu na amewachukua mimba katika aibu. Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu, ambao hunipa chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
for to fornicate mother their be ashamed to conceive them for to say to go: went after to love: lover me to give: give food: bread my and water my wool my and flax my oil my and drink my
6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake kwa vichaka vya miiba, nitamjengea ukuta ili kwamba asiweze kutoka.
to/for so look! I to hedge [obj] way: journey your in/on/with thorn and to wall up/off [obj] wall her and path her not to find
7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata; atawatafuta lakini hatawapata. Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza, kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi kuliko sasa.’
and to pursue [obj] to love: lover her and not to overtake [obj] them and to seek them and not to find and to say to go: went and to return: return to(wards) man: husband my [the] first for be pleasing to/for me then from now
8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta, niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia kwa kumtumikia Baali.
and he/she/it not to know for I to give: give to/for her [the] grain and [the] new wine and [the] oil and silver: money to multiply to/for her and gold to make: offer to/for Baal
9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari. Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
to/for so to return: return and to take: take grain my in/on/with time his and new wine my in/on/with meeting: time appointed his and to rescue wool my and flax my to/for to cover [obj] nakedness her
10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake mbele ya wapenzi wake; hakuna yeyote atakayemtoa mikononi mwangu.
and now to reveal: uncover [obj] lewdness her to/for eye: seeing to love: lover her and man: anyone not to rescue her from hand: power my
11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote: sikukuu zake za mwaka, sikukuu za Miandamo ya Mwezi, siku zake za Sabato, sikukuu zake zote zilizoamriwa.
and to cease all rejoicing her feast her month: new moon her and Sabbath her and all meeting: festival her
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema yalikuwa malipo yake kutoka kwa wapenzi wake; nitaifanya kuwa kichaka, nao wanyama pori wataila.
and be desolate: destroyed vine her and fig her which to say wages they(masc.) to/for me which to give: pay to/for me to love: lover me and to set: make them to/for wood and to eat them living thing [the] land: country
13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku alizowafukizia uvumba Mabaali; alipojipamba kwa pete na kwa vito vya thamani, na kuwaendea wapenzi wake, lakini mimi alinisahau,” asema Bwana.
and to reckon: punish upon her [obj] day [the] Baal which to offer: offer to/for them and to adorn ring her and jewelry her and to go: follow after to love: lover her and [obj] me to forget utterance LORD
14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi; nitamwongoza hadi jangwani na kuzungumza naye kwa upole.
to/for so behold I to entice her and to go: take her [the] wilderness and to speak: speak (upon *L(abh)*) heart her
15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu, nami nitalifanya Bonde la Akori mlango wa matumaini. Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama siku zile alizotoka Misri.
and to give: give to/for her [obj] vineyard her from there and [obj] Valley (of Achor) (Valley of) Achor to/for entrance hope and to answer there [to] like/as day youth her and like/as day to ascend: rise she from land: country/planet Egypt
16 “Katika siku ile,” asema Bwana, “utaniita mimi ‘Mume wangu’; hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
and to be in/on/with day [the] he/she/it utterance LORD to call: call by man: husband my and not to call: call by to/for me still Baal my
17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake, wala hataomba tena kwa majina yao.
and to turn aside: remove [obj] name [the] Baal from lip her and not to remember still in/on/with name their
18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani, na viumbe vile vitambaavyo ardhini. Upinde, upanga na vita, nitaondolea mbali katika nchi, ili kwamba wote waweze kukaa salama.
and to cut: make(covenant) to/for them covenant in/on/with day [the] he/she/it with living thing [the] land: country and with bird [the] heaven and creeping [the] land: soil and bow and sword and battle to break from [the] land: country/planet and to lie down: lay down them to/for security
19 Nitakuposa uwe wangu milele; nitakuposa kwa uadilifu na haki, kwa upendo na huruma.
and to betroth you to/for me to/for forever: enduring and to betroth you to/for me in/on/with righteousness and in/on/with justice and in/on/with kindness and in/on/with compassion
20 Nitakuposa kwa uaminifu, nawe utamkubali Bwana.
and to betroth you to/for me in/on/with faithfulness and to know [obj] LORD
21 “Katika siku ile nitajibu,” asema Bwana, “nitajibu kwa anga, nazo anga zitajibu kwa nchi;
and to be in/on/with day [the] he/she/it to answer utterance LORD to answer [obj] [the] heaven and they(masc.) to answer [obj] [the] land: country/planet
22 nayo nchi itajibu kwa nafaka, divai mpya na mafuta, navyo vitajibu kwa Yezreeli.
and [the] land: country/planet to answer [obj] [the] grain and [obj] [the] new wine and [obj] [the] oil and they(masc.) to answer [obj] Jezreel
23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitaonyesha pendo langu kwake yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’ Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’ ‘Ninyi ni watu wangu’; nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’”
and to sow her to/for me in/on/with land: country/planet and to have compassion [obj] not to have compassion and to say to/for not people my people my you(m. s.) and he/she/it to say God my

< Hosea 2 >