< Hosea 2 >

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
“Say to your brothers—Ammi, And to your sisters—Ruhamah.
2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni, kwa maana yeye si mke wangu, nami si mume wake. Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake na uzinzi kati ya matiti yake.
Plead with your mother—plead (For she [is] not My wife, and I [am] not her husband), And she turns her whoredoms from before her, And her adulteries from between her breasts,
3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa. Nitamfanya kama jangwa, nitamgeuza awe nchi ya kiu, nami nitamuua kwa kiu.
Lest I strip her naked. And have set her up as [in] the day of her birth, And have made her as a wilderness, And have set her as a dry land, And have put her to death with thirst.
4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake, kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
And her sons I do not pity, For they [are] sons of whoredoms,
5 Mama yao amekosa uaminifu na amewachukua mimba katika aibu. Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu, ambao hunipa chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
For their mother has gone whoring, Their conceiver has acted shamefully, For she has said, I go after my lovers, Those giving my bread and my water, My wool and my flax, my oil and my drink.
6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake kwa vichaka vya miiba, nitamjengea ukuta ili kwamba asiweze kutoka.
Therefore, behold, I am hedging up your way with thorns, And I have made a wall for her, And her paths she does not find.
7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata; atawatafuta lakini hatawapata. Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza, kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi kuliko sasa.’
And she has pursued her lovers, And she does not overtake them, And has sought them, and does not find [them], And she has said: I go, and I return to my first husband, For—better to me then than now.
8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta, niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia kwa kumtumikia Baali.
And she did not know that I had given to her The grain, and the new wine, and the oil. Indeed, I multiplied silver to her, And the gold they prepared for Ba‘al.
9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari. Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
Therefore I return, And I have taken My grain in its season, And My new wine in its appointed time, And I have taken away My wool and My flax, covering her nakedness.
10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake mbele ya wapenzi wake; hakuna yeyote atakayemtoa mikononi mwangu.
And now I reveal her dishonor before the eyes of her lovers, And none deliver her out of My hand.
11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote: sikukuu zake za mwaka, sikukuu za Miandamo ya Mwezi, siku zake za Sabato, sikukuu zake zote zilizoamriwa.
And I have caused all her joy to cease, Her festival, her new moon, and her Sabbath, Even all her appointed times,
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema yalikuwa malipo yake kutoka kwa wapenzi wake; nitaifanya kuwa kichaka, nao wanyama pori wataila.
And made desolate her vine and her fig tree, Of which she said, They [are] a wage to me, That my lovers have given to me, And I have made them for a forest, And a beast of the field has consumed them.
13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku alizowafukizia uvumba Mabaali; alipojipamba kwa pete na kwa vito vya thamani, na kuwaendea wapenzi wake, lakini mimi alinisahau,” asema Bwana.
And I have charged on her the days of the Ba‘alim, To whom she makes incense, And puts on her ring and her ornament, And goes after her lovers, And forgot Me,” a declaration of YHWH.
14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi; nitamwongoza hadi jangwani na kuzungumza naye kwa upole.
“Therefore, behold, I am enticing her, And have caused her to go to the wilderness, And I have spoken to her heart,
15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu, nami nitalifanya Bonde la Akori mlango wa matumaini. Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama siku zile alizotoka Misri.
And given to her her vineyards from there, And the Valley of Achor for an opening of hope, And she has responded there as in the days of her youth, And as in the day of her coming up out of the land of Egypt.
16 “Katika siku ile,” asema Bwana, “utaniita mimi ‘Mume wangu’; hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
And it has come to pass in that day,” A declaration of YHWH, “You call Me: My husband, And do not call Me anymore: My lord.
17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake, wala hataomba tena kwa majina yao.
And I have turned aside the names of the lords from her mouth, And they are not remembered anymore by their name.
18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani, na viumbe vile vitambaavyo ardhini. Upinde, upanga na vita, nitaondolea mbali katika nchi, ili kwamba wote waweze kukaa salama.
And I have made a covenant for them in that day, With the beast of the field, And with the bird of the heavens, And the creeping thing of the ground, And bow, and sword, and war I break from off the land, And have caused them to lie down confidently.
19 Nitakuposa uwe wangu milele; nitakuposa kwa uadilifu na haki, kwa upendo na huruma.
And I have betrothed you to Me for all time, And betrothed you to Me in righteousness, And in judgment, and kindness, and mercies,
20 Nitakuposa kwa uaminifu, nawe utamkubali Bwana.
And betrothed you to Me in faithfulness, And you have known YHWH.
21 “Katika siku ile nitajibu,” asema Bwana, “nitajibu kwa anga, nazo anga zitajibu kwa nchi;
And it has come to pass in that day, I answer,” A declaration of YHWH, “I answer the heavens, and they answer the earth.
22 nayo nchi itajibu kwa nafaka, divai mpya na mafuta, navyo vitajibu kwa Yezreeli.
And the earth answers the grain, And the new wine, and the oil, And they answer Jezreel.
23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitaonyesha pendo langu kwake yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’ Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’ ‘Ninyi ni watu wangu’; nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’”
And I have sowed her to Me in the land, And I have pitied Lo-Ruhamah, And I have said to Lo-Ammi, You [are] My people, And he says, My God!”

< Hosea 2 >