< Hosea 2 >

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
Kald eders Broder Mit-Folk og eders Søster nåderig.
2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni, kwa maana yeye si mke wangu, nami si mume wake. Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake na uzinzi kati ya matiti yake.
Gå i rette med eders Moder, gå i rette, thi hun er ikke min Hustru, og jeg er ej hendes Mand. For Hormærket fri hun sit Ansigt, for Bolemærket sit Bryst.
3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa. Nitamfanya kama jangwa, nitamgeuza awe nchi ya kiu, nami nitamuua kwa kiu.
Jeg klæder hende ellers nøgen, stiller hende frem, som hun fødtes; jeg reder hende til som en Ørk, som et Tørkeland gør jeg hende, lader hende tørste ihjel.
4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake, kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
Jeg ynkes ej over hendes Børn, fordi de er Horebørn;
5 Mama yao amekosa uaminifu na amewachukua mimba katika aibu. Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu, ambao hunipa chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
thi Horkvinde var deres Moder, skamløs var hun, som bar dem. Thi hun sagde: "Mine Elskere holder jeg mig til, som giver mig mit Brød og mit Vand, min Uld og min Hør, min Olie og Vin."
6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake kwa vichaka vya miiba, nitamjengea ukuta ili kwamba asiweze kutoka.
Se, derfor spærrer jeg med Tjørn hendes Vej, foran hende murer jeg en Mur, så hun ikke kan finde sine Stier.
7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata; atawatafuta lakini hatawapata. Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza, kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi kuliko sasa.’
Efter Elskerne kan hun så løbe, hun når dem alligevel ikke; hun søger dem uden at finde, og da skal hun sige: "Jeg går på ny til min første Mand; da, havde jeg det bedre end nu."
8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta, niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia kwa kumtumikia Baali.
Ja hun, hun skønner ikke, at det var mig, som gav hende Korn og Most og Olie, gav hende rigeligt Sølv. og Guld, som de gjorde til Baaler.
9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari. Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
Derfor tager jeg atter mit Korn, når Tiden er til det, min Most, når Timen er inde, borttager min Uld og min Hør, som hun skjuler sin Nøgenhed med.
10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake mbele ya wapenzi wake; hakuna yeyote atakayemtoa mikononi mwangu.
Jeg blotter nu hendes Skam lige for Elskernes Øjne, af min Hånd frier ingen hende ud.
11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote: sikukuu zake za mwaka, sikukuu za Miandamo ya Mwezi, siku zake za Sabato, sikukuu zake zote zilizoamriwa.
Jeg, gør Ende på al hendes. Glæde, Fester, Nymåner, Sabbater, hver en Højtid, hun har.
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema yalikuwa malipo yake kutoka kwa wapenzi wake; nitaifanya kuwa kichaka, nao wanyama pori wataila.
Jeg ødelægger hendes Vinstok og Figentræ, om hvilke hun sagde: "Her er min Skøgeløn, den, mine Elskere gav mig." Jeg skaber dem om til Krat, af Markens Dyr skal de ædes.
13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku alizowafukizia uvumba Mabaali; alipojipamba kwa pete na kwa vito vya thamani, na kuwaendea wapenzi wake, lakini mimi alinisahau,” asema Bwana.
Jeg hjemsøger hende for Baalernes Fester, på hvilke hun bragte dem Ofre, smykket med Ring og Kæde. Sine Elskere holdt hun sig til, mig glemte hun, lyder det fra HERREN.
14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi; nitamwongoza hadi jangwani na kuzungumza naye kwa upole.
Se, derfor vil jeg lokke og føre hende ud i Ørkenen og tale hende kærligt til.
15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu, nami nitalifanya Bonde la Akori mlango wa matumaini. Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama siku zile alizotoka Misri.
Så giver jeg hende hendes Vingårde der og Akors Dal til en Håbets Dør. Der skal hun synge som i Ungdommens Dage, som da hun drog op fra Ægyptens Land.
16 “Katika siku ile,” asema Bwana, “utaniita mimi ‘Mume wangu’; hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
På hin Dag, lyder det fra HERREN, skal hun påkalde sin Ægtemand, og ikke mere Baalerne.
17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake, wala hataomba tena kwa majina yao.
Baalsnavnene fjerner jeg fra hendes Mund, ej mer skal Navnene huskes.
18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani, na viumbe vile vitambaavyo ardhini. Upinde, upanga na vita, nitaondolea mbali katika nchi, ili kwamba wote waweze kukaa salama.
På hin Dag slutter jeg en Pagt for dem med Markens Dyr og Himmelens Fugle og Jordens Kryb; Bue, Sværd og Stridsvåben sønderbryder jeg i Landet, og jeg lader dem bo trygt.
19 Nitakuposa uwe wangu milele; nitakuposa kwa uadilifu na haki, kwa upendo na huruma.
Jeg trolover mig med dig for evigt, jeg trolover mig med dig med Retfærd og Ret, med Miskundhed og Barmhjertighed;
20 Nitakuposa kwa uaminifu, nawe utamkubali Bwana.
jeg trolover mig med dig i Troskab, og du skal kende HERREN.
21 “Katika siku ile nitajibu,” asema Bwana, “nitajibu kwa anga, nazo anga zitajibu kwa nchi;
Da skal det ske på hin Dag, at jeg bønhører, lyder det fra HERREN, ja, at jeg bønhører Himlen, at den så bønhører Jorden,
22 nayo nchi itajibu kwa nafaka, divai mpya na mafuta, navyo vitajibu kwa Yezreeli.
og Jorden bønhører Hornet, Mosten og Olien, og de bønhører Jizreel.
23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitaonyesha pendo langu kwake yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’ Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’ ‘Ninyi ni watu wangu’; nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’”
Jeg sår hende ud i Landet, mod Nådeløs er jeg nådig og siger til Ikke-mit-Folk: "Mit Folk er du!" og han skal sige: "Min Gud!"

< Hosea 2 >