< Hosea 13 >

1 Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka, alikuwa ametukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali naye akafa.
Quand Ephraïm a parlé, il y a eu des tremblements. Il s'est exalté en Israël, mais quand il s'est rendu coupable par Baal, il est mort.
2 Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
Maintenant, ils pèchent de plus en plus, et se sont fait des images en fonte de leur argent, même des idoles selon leur propre compréhension, tous sont le fruit du travail des artisans. On dit d'eux: « Ils offrent des sacrifices humains et embrassent les veaux.
3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
C'est pourquoi ils seront comme la brume du matin, comme la rosée qui disparaît tôt, comme l'ivraie qu'un tourbillon chasse de l'aire de battage, et comme la fumée qui sort de la cheminée.
4 “Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
« Pourtant, je suis Yahvé, ton Dieu, depuis le pays d'Égypte; et vous ne reconnaîtrez aucun autre dieu que moi, et à part moi, il n'y a pas de sauveur.
5 Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
Je t'ai connu dans le désert, dans le pays de la grande sécheresse.
6 Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
Ils ont été rassasiés selon leurs pâturages; ils ont été rassasiés, et leur cœur a été exalté. C'est pourquoi ils m'ont oublié.
7 Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
C'est pourquoi je suis pour eux comme un lion. Comme un léopard, je vais me cacher sur le chemin.
8 Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
Je les rencontrerai comme une ourse qui se languit de ses petits, et déchirera la couverture de leur cœur. Là, je les dévorerai comme une lionne. L'animal sauvage va les déchirer.
9 “Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
Tu es détruit, Israël, parce que tu es contre moi, contre votre aide.
10 Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
Où est maintenant ton roi, pour qu'il te sauve dans toutes tes villes? Et vos juges, dont vous avez dit: « Donnez-moi un roi et des princes »?
11 Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
Je vous ai donné un roi dans ma colère, et je l'ai emmené dans ma colère.
12 Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
La culpabilité d'Ephraïm a été mise en réserve. Son péché est stocké.
13 Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
Les douleurs d'une femme en travail l'atteindront. C'est un fils imprudent, car quand le moment est venu, il ne vient pas à l'ouverture des entrailles.
14 “Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol h7585)
Je les rachèterai de la puissance du séjour des morts. Je les rachèterai de la mort! Mort, où sont tes fléaux? Sheol, où est ta destruction? « La compassion sera cachée à mes yeux. (Sheol h7585)
15 hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
Bien qu'il soit fécond parmi ses frères, un vent d'est viendra, le souffle de Yahvé qui monte du désert; et sa source deviendra sèche, et sa fontaine sera tarie. Il pillera l'entrepôt du trésor.
16 Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”
La Samarie portera sa culpabilité, car elle s'est rebellée contre son Dieu. Ils tomberont par l'épée. Leurs enfants seront mis en pièces, et leurs femmes enceintes seront éventrées. »

< Hosea 13 >